MICHEPUKO NOMA: ACHANWA NA VYEMBE NA KUTEMBEZWA UMBALI WA MITA 300 BILA NGUO MCHANA KWEUPE MTAA WA MSAMVU B KIHONDA MAGHOROFANI MKOANI MOROGORO

Aliyekatwa nyembe.
MWANAMKE mmoja,  Rehema Juma (21) ambaye ni mke wa mtu, mkazi wa Mtaa wa Msamvu B, Kata ya Kihonda Maghorofani mkoani Morogoro amechanwa na nyembe mwilini na baadaye kutembezwa bila nguo mtaani mchana kweupe akituhumiwa kufumwa na mume wa mtu.Tukio hilo la aina yake  ambalo lilivuta umati mkubwa, lilitokea Julai 5, mwaka huu saa 10 jioni katika Mtaa wa Msamvu B.Mashuhuda wa tukio hilo walipohojiwa na paparazi walidai kuwa kwa muda mrefu, Zaitun Ally (30) ambaye pia anaishi kwenye mtaa huo alikuwa akimshutumu Rehema akidai anatembea na mumewe, hivyo akaamua kutega mtego bila mafanikio.“Zaituni baada ya kushindwa kuwanasa leo aliamua kumuita Rehema nyumbani kwake na kudai amewafuma na mumewe hivyo kumchana nyembe baadaye kumvua nguo na kumtembeza bila nguo mtaani hadi nyumbani kwake umbali wa mita 300 mchana kweupe,” alisema mmoja wa mashuhuda hao aliyejitambulisha kwa jina la Ashura Ally.
Rehema Juma akiwa na mama yake.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.