Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2016

Sergio Ramos alivyozuia rekodi ya Real Madrid isivunjwe na FC Barcelona Dec 3 2016

Picha
Baada ya presha na ubishi wa zaidi ya wiki moja wa mashabiki wa FC Barcelona na Real Madrid za Hispania , kubishana timu ipi itapata ushindi katika mchezo wa El Clasico uliochezwa katika uwanja wa Nou Camp jijini Barcelona , hatimae ubishi umemalizwa usiku wa December 3 2016. Timu za Barcelona na Real Madrid zote ziliingia zikiwa na kumbukumbu kuwa mchezo wao wa mara ya mwisho kumalizika pasipo goli ilikuwa ni mwaka 2002, huku Real Madrid waliingia kutetea rekodi yao ya kucheza mechi yao ya 33 bila kuruhusu kupoteza mchezo hata mmoja na kutoka sare mechi 6 pekee. December 3 2016 katika uwanja wa Nou Camp mchezo huo wa El Clasico umemalizika kwa sare ya kufungana goli 1-1, FC Barcelona ndio walikuwa wa kwanza kupata goli dakika ya 53 kupitia kwa Luis Suarez na Real Madrid wakafanikiwa kusawazisha goli dakika ya 90 kupitia kwa Sergio Ramos . Msimamo wa LaLiga baada ya matokeo ya mechi ya FC Barcelona vs R

MAMBO Yanayoshusha Thamani ya Mwanaume Mbele ya Mwanamke

Picha
Katika uhusiano baina ya mume na mke hutokea mambo mbalimbali yanayoimarisha uhusiano baina yao au kuuharibu. Baadhi ya nyakati mwanaume hufanya baadhi ya mambo yanayomshusha thamani mbele ya mwanamke. Hivyo, wanaume wote wenye khofu ya heshima na thamani yao kuanguka, ninawaletea mambo muhimu ambayo yanashusha thamani ya mwanaume mbele ye mwanamke: 1. HADAA NA UNYONYAJI: Baadhi ya wanaume ni wazuri sana katika kumnyonya mwanamke kwa kutumia kisingizio cha mapenzi. Wanazitumia mali zake na kuzinyonya kwa kutumia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na maneno matamu ya mapenzi au kutengeneza simulizi za uongo kuhusu matatizo ya kipesa na kiuchumi. Mwanamke akigundua kuwa analaghaiwa, basi atamshusha thamani haraka mwanaume huyo na kuamua kujitenga naye. Na iwapo ataendelea kuwa naye, basi hasara na majuto yatakuwa juu ya mwanamke huyo. 2. WANAWAKE WENGI: Mwanamke anapenda ahisi kuwa yeye ndiye mtu pekee katika maisha ya mwanaume. Kuwa na uhusiano na wana

BONGO Movie Yazidi Kufa, JB Nae Aacha Kuigiza

Picha
Msanii wa siku nyingi wa bongo movie JB amestaafu kuigiza bongo movie, hii imesikitisha sana wadau wa sanaa, kuanzia mashabiki hadi wasanii wenzake..

TAHARUKI...Panya Road Wavamia Nyumba na Kupora..Majirani Washindwa Kusaidia

Picha
DAR: Kundi kubwa la vijana wanaosadikika kuwa ni 'Panya Road' wavamia nyumba moja na kupora vitu mbalimbali usiku wa kuamkia leo. Inadaiwa kuwa mhanga wa tukio hilo alijaribu kuomba msaada kwa majirani bila mafanikio kwakuwa majirani hao waliogopa kutoka na kupambana na Panya Road hao. Mmoja wa majirani amenukuliwa akisema kuwa Vijana hao walikuwa na Mapanga Marungu, Jambia na Baruti walizokuwa wakizilipua ili kutisha watu kuwa ni Risasi.

SALAMU za Rambirambi za Rais Magufuli Kufuatia Kifo cha Rais Mstaafu wa Cuba, Fidel Castro

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli, amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Raul Castro kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Cuba Mhe. Fidel Castro kilichotokea tarehe 25 Novemba, 2016. Katika Salamu hizo Rais Magufuli amesema; "Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Fidel Castro. Kwa niaba ya Serikali, Wananchi wa Tanzania na kwa niaba yangu mwenyewe natoa pole nyingi kwako, familia, Serikali ya Cuba na wananchi wa Cuba kwa kumpoteza mtu muhimu. Fidel Castro alikuwa kiongozi shupavu wa karne, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika na pia kwa misaada mikubwa aliyoitoa katika kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi. Alikuwa rafiki wa Tanzania na Afrika nzima, historia ya Tanzania na Afrika haziwezi kukamilika bila kumtaja Fidel Castro, hakika kifo chake sio tu ni pigo kwa Cuba bali pia kwa Tanzania na Afrik

KIMENUKA..Kura za Urais Kuhesabiwa Upya Marekani

Picha
Tume ya uchaguzi katika jimbo la Wisconsin nchini Marekani limepokea ombi la kurudiwa kuhesabu kura za uchaguzi uliopita ambapo mshindi alikuwa Donald Trump aliyeshinda kwa kura chache wiki mbili zilizopita. Ombi la kurudiwa kuhesabu kura liliwasilishwa na mgombea wa urais kupitia chama cha  Green Party Jill Stein ambaye pia ametaka kura zirudiwe kuhesabiwa katika majimbo ya  Michigan na Pennsylvania. Hata hivyo ikiwa Hillary Clinton atashinda jimbo hilo hakutabadilisha matokeo ya ushindi wa Trump kwani lina kura 10 pekee za wajumbe wa uchaguzi.  Kamisheni hiyo imethibitisha kupokea maombi hayo na kuainisha kutoa maelekezo muda si mrefu.

KUFUATIA Agizo la Waziri wa Elimu Wanafanzi wa IFM Wavuliwa Majoho Katikati ya Mahafali

Picha
Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kimeanza utekelezaji wa agizo la Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, kwa kuwazuia wahitimu wa ngazi ya cheti na stashahada kuvaa majoho na kofia wakati wa mahafali yao. Kitendo hicho kilitokea katika Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam juzi baada ya mratibu wa mahafali ya 42 ya IFM, Dk. Godwin Kaganda, kutangaza utaratibu huo licha ya wahitimu wao kuvaa majoho yao. Dk. Kaganda alisema utaratibu huo ni kwa mujibu ya miongozo iliyotolewa na Serikali kuhusu uvaaji wa majoho, ambao unataka yavaliwe na wahitimu wa kuanzia ngazi ya shahada na kuendelea. “Wahitimu wote wa ngazi ya cheti na stashahada hamtovaa majoho wala kofia pamoja na kwamba mlishapewa awali, tunaomba radhi kwa sababu ndiyo miongozo tuliyopewa,” alisema Dk. Kaganda. Wiki iliyopita, Profesa Ndalichako  alipokuwa akiwatunuku vyeti wahitimu wa mafunzo ya uongozi na usimamizi wa elimu kwa njia ya masafa, ili

Soyinka: Nitaondoka Marekani Trump akiapishwa

  Mshindi wa Tuzo la Nobel na mwandishi raia wa Nigeria Wole Soyinka, anasema kuwa ataondoka Marekani siku ambayo Donald Trump ataapishwa kuwa rais. Wiki iliyopita Soyinka aliahidi kuwa angeirarua green Card yake, ikiwa Trump angechaguliwa kuwa rais wa Marekani. Green Card humpa mtu kibali ya kuishi rasmi nchini Marekani na hupewa umuhimu mkubwa na wahamiaji kutoka nchi za Afrika. Soyinka alitoa matamshi hayo wakati akihutubia wanafunzi katika chuo cha Oxford nchini Uingereza. Mwandishi huyo maarufu alionekana kuchukua msimamo mkali kupinga seza za uhamiaji za bwana Trump. Soyinka alishinda tuzo la Nobel la fasihi mwaka 1986 na kuwa mwafrika wa kwanza kupata tuzo hilo.

Trump awasili White House

Rais mteule wa Marekani Donald Trump amewasili katika Ikulu ya White House, kwa mujibu wa maafisa nchini Marekani. Hata hivyo aliingia akitumia mlango tofauti na kuwasili kwake hakukunaswana kamera za waandishi wa habari. Anatarajiwa kuwa kwenye mazungumzo na Rais Obama wakati huu. Licha ya tofauti zao, bwana Obama siku ya Jumatano alikishauri kikosi chake kufanya jitihada zaidi kuhakisha kuwa kuna mafanikio kwenye shughuli ya kupokeza madaraka kwa Republican mwezi Januari. Image caption Waandishi wa habari wakimsubiri Trump White House Mapema kikosi cha kampeni ya Trump kilikutana na washauri kujadili masuala kuhusu siku za kwanza 100 za Trump kama rais na ut

Ushauri kwa Mabinti wa Makamo Wenye Kiu na Ndoa.....

Picha
Leo nimeona nije hadharani hapa kutoa ushauri kwa mabinti wa makamo (30+yrs) ambao huenda kwa sababu za hapa na pale hawajafanikiwa kuingia kwenye ndoa wala kuwa na mahusiano yanayoashiria kuanzisha familia hivi karibuni. Msingi wa mada yangu umetokana na mabinti kadhaa ninao kutana nao mara kwa mara maeneo mbali mbali kuwa na vilio karibu sawa. Wakati nafanya kazi Taasisi fulani Dsm, kuna dada nilizoena nae kiasi cha kunisimulia baadhi ya mikasa ya kimahusiano na changamoto anazopitia. Binti huyo mwenye miaka zaidi ya 30 alipitia magumu ikiwa ni pamoja na kutoa mimba kadhaa baada ya kutoona mwelekeo wa waliompachika, kuamua kugharamia mahusiano kwa kumuhudumia kila kitu mwanaume, kulazimika kubadili dini mara kadhaa kwa ajili ya mwanaume Ki uficho bila wazazi wala ndugu zake kujua. Yote hayo aliyafanya ili kuwaridhisha wanaume angalau aitwe Mke wa fulani!! Lakini cha ajabu alikuwa anaambulia patupu Si huyo tu, wako wengi wa namna hiyo na ambao wa

Jay Dee Atiwa Hatiani, Atakiwa Amuombe Radhi Ruge wa Clouds FM

Picha
Mahakama ya Wilaya Kinondoni imemtia hatiani mwanamuziki nyota wa kike nchini Judith Wambura (Lady Jay Dee) kwa kutoa maneno ya kashfa dhidi ya Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba.Tokeo la picha la lady jaydee Mahakama hiyo imemuamuru aombe radhi kupitia kwenye chombo cha habari chenye "coverage" pana nchini kote na ikiwezekana duniani. Katika hati ya madai hayo, mwanamuziki huyo anashtakiwa na viongozi wa Clouds Media Group ambao ni Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga kwa kuuchafua uongozi wa kampuni hiyo na viongozi wake kupitia mitandao ya kijamii katika malumbano makali kati ya pande hizo mbili. Mei 2013, Clouds Media Group na Ruge walimburuza Jay Dee mahakamani kwa kile walichodai kwamba alikuwa akiwatukana kwenye mitandao ya kijamii.

undani wa Msichana huyu Aliyebakwa Hadi Kufa – Makumira University

Picha
Mapema jana zimesambaa Picha kwenye Mitandao ya kijamii ikimuonyesha Msichana anayefahamika kwa jina la JULIANA ISAWAFO Ambaye Amebakwa hadi Kufa na Kutupwa Nje ya eneo la Chuo Kikuu cha Tumaini (Makumira Arusha). Mmoja wa Viongozi wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo hicho ambapo amethibitisha kwamba ni kweli Ameokotwa Msichana huyo Majira ya Saa tano asubuhi ya Leo akiwa Amekufa na mwili wake Kutelekezwa kwenye Shamba la Mpunga hatua chache nje ya Eneo la Chuo. Hata hivyo Amenithibitishia kwamba Msichana huyo ni Mwanafamilia wa Chuo cha Makumira ila sio Mwanafunzi rasmi kama watu wanavyodai. Anasema Msichana huyo alikuwa akiishi ndani ya eneo la Chuo kwa Mzungu mmoja ambaye ni mmoja wa waalimu wa Sanaa Chuoni hapo. Hata hivyo hakusita kuweka wazi kwamba Wanasikitika sana Kwa Tukio hilo kwani Msichana huyo alikuwa kama Dancer wa Matamasha ya Chuo cha Makumira.

Taarifa Kutoka Ikulu: Rais Magufuli na Rais Kenyatta Wazindua Barabara ya Southern By-pass

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta leo tarehe 01 Novemba, 2016 wamezindua barabara ya Southern By-pass iliyojengwa kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Nairobi nchini Kenya. Sherehe ya uzinduzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 28 na inayounganisha maeneo mbalimbali ya Jiji la Nairobi imefanyika katika eneo la Karen nje kidogo ya Jiji la Nairobi. Akizungumza katika sherehe hiyo Rais Magufuli amempongeza Rais Kenyatta na Serikali yake kwa kujenga barabara hiyo ambayo sio tu itawasaidia wananchi wa Kenya bali pia itawasaidia wananchi wa Afrika Mashariki wanaotumia barabara zinazopitia Nairobi. Rais Magufuli pia ameishukuru Serikali ya China kupitia benki yake ya Exim ambayo imetoa mkopo wa kujenga barabara hiyo, kwa kuendelea kuziamini nchi za Afrika Mashariki na kuzikopesha mikopo inayosaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa

Kamati ya Bunge Yakataa faini ya 500,000/- Kwa Kila Kosa Barabarani

Picha
Kamati  ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala imekataa mapendekezo ya kufanyia marekebisho Sheria ya Leseni za Uchukuzi ya mwaka 1973 yenye lengo la kuongeza kiwango cha adhabu ya faini hadi kufikia asilimia 500 kwa watakaokiuka masharti ya leseni hizo. Mapendekezo hayo yaliwasilishwa mbele ya kamati hiyo mjini Dodoma jana na Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra). Baada ya kuyakataa mapendekezo hayo, kamati hiyo imetoa muda wa siku mbili kwa Sumatra kuhakikisha inawasilisha mbele ya kamati hiyo mapendekezo yanayokubalika. Sumatra inapendekeza kuongeza kiwango cha adhabu ya faini kutoka kati ya Sh 10,000 na Sh 50,000 hadi Sh 200,000 na 500,000 kwa watoa huduma za uchukuzi, watakaokiuka masharti ya leseni zao. Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohammed Mchengerwa alisema mapendekezo hayo, yatazidi kuwaongezea mzigo Watanzania badala ya kuwasaidia. Alisema kiwango hicho cha faini kubwa, kamwe hakitazuia tatizo la ajali za barabarani, zaidi ya

Wema Sepetu Awashukuru Waliomtumia Salamu za Birthday

Picha
Jumatano hii ilikuwa ni siku ya kuzaliwa ya staa wa filamu Wema Sepetu ambao ndugu, jamaa pamoja na marafiki walimtakia heri na mafanikio mrembo huyo. Moja kati ya vitu ambavyo vilileta gumzo kwenye mitandao ya kijamii ni baada ya mama Diamond kum-wish malkia huyo wa filamu huku akimkaushia Zari ambaye ni mama watoto wa Diamond. Pia dada zake na Diamond walim-wish maklia huyo. Baada ya kupokea salamu za watu mbalimbali kutoka katika kila kona ya dunia malkia huyo wa filamu na yeye aliamua kuwashurudu huku akionyesha kile ambacho hakukitarajia. Wema kupitia istagram aliandika: Wow… wow… wow… daah.. sijui cha kuandika.. am just out of words… Wema mimi nitamlipa nini Mungu kwa Neema na Baraka zake anazonijalia kila siku…?? Napenda kutoa shukrani zangu za Dhati kwa mumumu wangu, My family, my management, teamkazi wale kwa kufungua dimba last Night with that amazing suprise… alafu sasa huku insta, snapchat, twitter and kila site ambazo mmepost about M

Prof. Lipumba: Sing'oki ng'o. Mimi ni Mwenyekiti halali CUF, Kikao kilichonivua uanachama ni batili

Picha
Katika mahojiano na sauti ya Amerika VOA Swahili jana jioni, Mwenyekiti aliyejiuzulu wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba amesema kuwa yeye bado ni Mwenyekiti halali na kikao kilichomvua uanachama ni batili. Akihojiwa na mwandishi wa habari mahiri Sunday Shomari, Mwenyekiti huyo aliyejiuzulu amesisitiza kuwa yeye bado ni mwenyekiti halali kwa mujibu wa katiba ya CUF na kikao kilichoongozwa na Mhe. Katani huko Unguja ni batili na yeye anaendelea na shughuli za kichama kama kawaida.

ZARI Amuumbua Hamisa Mobetto, Aanika Live Uchafu Wake na Diamond

Picha
Zile tetesi za muda mrefu kuhusu mwanamuziki Diamond Platnums pamoja model maarufu nchini, Hamisa mobeto aka Salome kuvunja amri ya sita huenda zikazaa matunda soon baada ya hivi karibuni mzazi mwenzie ,ambaye pia ni mpenzi wake wa sasa, Zari Hassan ambapo kupitia page yake ya snapchat amepost picha za hereni huku zikiwa zimeambata na ujumbe mzito, ambapo alimtaka mwenye hereni hizo cheap alizozisahau chumbani kwake akazichukue mara moja. Hata hivo kwa mujibu wa wapenda umbea mjini aka team chambua kama karanga waliweza kuzichambua hereni hizo vizuri na kubaini kuwa zilishawahi kuvaliwa na mwanamitindo maarufu nchini Hamisa Mobetto(pichani) aka SALOME. Huenda hii ikawa habari Kali kwa wiki hii, hata hivyo bado Zari hajafunguka chochote kuhusu mmliki wa hereni hizo, wala Hamisa bado hajazungumzia chochote kama ni kweli uchafu huo (kama alivyoita Zari) ni wake au sio

TCRA Yadai Haipendi Kufungia vyombo vya Habari ila Sheria Inawalazimu

Picha
Mamlaka ya Mawasiliano ya Tanzania, TCRA, imesema haifurahii kuvifungia vyombo vya habari bali inavitaka vifuate kanuni na sheria zilizopo. Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA, Joseph Mapunda, ameyasema hayo akiwa jijini Mbeya. “Hatufurahii vyombo kufungwa, hatufurahii vyombo kupewa adhabu,lengo kubwa ni kuvifanya vyombo viwajibike, kwa mujibu wa sheria viwajibike pia kwa wananchi,viwajibike kwa nchi,” alisema. “Tunasajili vyombo vingi ili viweze kusaidia, kuhamasisha, kuelimisha, na kuhabarisha wananchi sasa litakuwa halina maana,” aliongeza. Hivi karibuni kamati hiyo ilikifungia kwa miezi mitatu kituo cha redio cha Radio 5.

JK Afanya ‘Ukauzu’ Ughaibuni

Picha
RAIS Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, amekataa kuzungumza na waandishi wa habari mjini New York, Marekani huku msaidizi wake akiwapiga vikumbo waandishi hao ili wasimsumbue ‘bosi’ wake, baada ya kutoka katika mkutano wa 71 wa Umoja wa Mataifa, anaandika Charles William. Mkutano huo ulioanza jana mjini New York, unajadili masuala mbalimbali ikiwemo vita dhidi ya ugaidi pamoja na utolewaji wa misaada zaidi kwa wakimbizi. Mkanda wa video uliopatikana leo, umemuonyesha Dk. Kikwete akitoka katika eneo la mkutano huku wandishi wa habari wakijaribu kumuhoji lakini akikataa na kuendelea kutembea, akiondoka katika eneo hilo. Baada ya Dk. Kikwete kukataa kuhojiwa alionekana akiwatupia maneno waandishi hao. Hata hivyo maneno hayo hayakuweza kunaswa na vinasa sauti vya wandishi hao huku msaidizi wake akiwazuia waandishi hao ili wasiendelee kumsogelea. Haikujulikana mara moja, kwanini Dk. Kikwete alikataa kuzungumza na wandishi wa habari katika eneo la nje ya mkut

MATOKEO YAMPA KIBURI GUARDIOLA, AINGIA MTAANI NA KUJIACHIA NA MKEWE

Picha
  Sasa ulitaka afanye mini? Maana Kocha wa Man City, Pep Guardiola mambo yanamuendea vizuri naye ameamaua kujiachia kiana. jana asubuhi  alionekana akiwa  katikati ya mitaa ya  jiji la Manchester akijiachia na mkewe Cristina Serra. Pamoja na mkewe, Guardiola, kocha wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich aliongoza na kocha wa viungo ambaye ni memba wa benchi lake, Lorenzo Buenaventura. Mwendo wa kikosi cha Man City chini yake unaonyesha uko safi na tayari ameanza kupewa nafasi ya kubeba ubingwa wa Ligi Kuu England

Polisi Marekani Yamkamata Mshukiwa wa Shambulio

Picha
Mtu aliyekuwa akitafutwa kuhusiana na mashambulio ya mabomu katika miji ya New York na New Jersey amekamatwa baada ya kushambuliana na polisi kwa risasi. Ahmed Khan Rahami, mwenye umri wa miaka 28 ni raia wa Marekani mwenye asili ya Afghan. Alijeruhiwa katika mapambano hayo yaliyosababishwa kukamatwa kwake karibu na nyumba yake kwenye mji wa New Jersey. Katika operesheni ya kumkamata mtuhumiwa huyo polisi wawili pia walijeruhiwa. Meya wa mji wa New York, Bill de Blasio amesema kuna kila sababu kuamini kwamba shambulio hilo lilikuwa ni ugaidi. Kwa upande wake Rais Barack Obama amewataka watu kuwa watulivu na kuongeza kuwa kila mtu ana mchango katika kuondoa hali hiyo.

ZITTO, Kafulila Wamtwisha Mzigo wa Escrow Rais Magufuli

Picha
Wakati Baraza la Usuluhishi la Benki ya Dunia likitoa hukumu ya kutaka Tanesco kuilipa Benki ya Standard Chartered-Hong Kong (SCB-HK) Sh320 bilioni, wanasiasa wawili walioibua sakata hilo bungeni wamechachamaa wakimtaka Rais John Magufuli awafikishe mahakamani wote waliohusika katika sakata la escrow. Katika hukumu hiyo, Baraza hilo limeitaka Tanesco kulipa mamilioni hayo ya fedha baada ya mgogoro wa muda mrefu kati yake na Kampuni ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL). Uamuzi huo umekuja wakati Serikali ilisharuhusu kufanyika kwa malipo ya Sh306 bilioni kutoka katika akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa imefunguliwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa ajili ya sakata hilo kwenda kwa kampuni ya Pan Africa Power Solutions (T) Ltd (PAP). Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Leila Muhaji alisema katika shauri hilo, shirika hilo liliwakilishwa na mawakili binafsi kutoka kampuni ya uwakili ya Rweyongeza na ndiyo itakayotoa taarifa kuhusu hukumu hiyo. Maoni y

TAARIFA RASMI KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA IKULU LEO

Picha
Tweet Tweet ? ? at 6:43 PM Email This

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Septemba 18

Picha
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Septemba 18

RAIS Magufuli: Tetemeko Halijaletwa na Serikali, Watu Wafanye Kazi

Picha
Mkuu Anasema waathirika wasikae tu huko wanangoja hela za serikali kwa sbb wanasikia zimechangwa,waanze kujisaidia kwanza wao na serikali itawasaidia pale waliposhindwa. Mkuu anasema mtu ukuta umedondoka, anataka asubiri serikali ndio imtengenezee! Watu wajue tetemeko ni janga la asili halijaletwa na CCM. Waanze kwa kujenga wenyewe kuta zilizodondoka sio wasubiri serikali, sababu maisha yanendelea na watu wanatakiwa wafanye kazi kwa kujenga nyumba zao na sio kila kitu serikali itafanya. Na wale wanasiasa wanaotaka kutumia janga hili kujinufaisha kisiasa mkuu anasema waache mara moja....Na kasema wote wanaotumia janga hili kukusanya misaada kwa njia ya kitapeli, basi wakamatwe mara moja.

Matembezi Dar yakusanya Sh1.5 bilioni za waathirika wa tetemeko Kagera

Picha
TAKRIBANI shilingi bilioni 1.5 zimechangwa kufuatia matembezi ya hisani yaliyopewa jina la “Walk for Kagera” yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kusaidia wahanga wa Tetemeko la Ardhi lililotokea tarehe 10 septemba mwaka huu mjini Bukoba Mkoani Kagera. Akizungumza mara baada ya matembezi hayo Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mhe Ally Hassan Mwinyi aliwashukuru wadau mbalimbali waliojitokeza na kushiriki matembezi hayo ya hisani. “Nawapongeza sana wadau wote mlioshiriki katika matembezi haya, mmeonyesha mshikamano mkubwa kwa umoja wenu mmeweza kuchangisha jumla ya shilingi 1,502,680,000 hii inatia faraja sana muendelee na moyo huo” Alisema Mzee Mwinyi. Kwa upande wake Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Kagera kuwa Serikali inafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wahanga wa tetemeko hilo wanapatiwa huduma stahiki na kwa wakati. Balozi Kijazi aliongeza kuwa kutokana na kuguswa na tatizo hilo Serikal