ZARI Amuumbua Hamisa Mobetto, Aanika Live Uchafu Wake na Diamond


Zile tetesi za muda mrefu kuhusu mwanamuziki Diamond Platnums pamoja model maarufu nchini, Hamisa mobeto aka Salome kuvunja amri ya sita huenda zikazaa matunda soon baada ya hivi karibuni mzazi mwenzie ,ambaye pia ni mpenzi wake wa sasa, Zari Hassan ambapo kupitia page yake ya snapchat amepost picha za hereni huku zikiwa zimeambata na ujumbe mzito, ambapo alimtaka mwenye hereni hizo cheap alizozisahau chumbani kwake akazichukue mara moja.

Hata hivo kwa mujibu wa wapenda umbea mjini aka team chambua kama karanga waliweza kuzichambua hereni hizo vizuri na kubaini kuwa zilishawahi kuvaliwa na mwanamitindo maarufu nchini Hamisa Mobetto(pichani) aka SALOME.

Huenda hii ikawa habari Kali kwa wiki hii, hata hivyo bado Zari hajafunguka chochote kuhusu mmliki wa hereni hizo, wala Hamisa bado hajazungumzia chochote kama ni kweli uchafu huo (kama alivyoita Zari) ni wake au sio

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.