Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2015

ZITTO KABWE ACHAFUA HALI YA HEWA ZANZIBAR,APEWA SIKU 14 KUOMBA RADHI LASIVYO KUPANDISHWA KIZIMBANI

Picha
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amepewa siku 14 kufuta kauli yake na kuomba radhi kwa kumhusisha rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na makosa ya uhaini. Msimamo huo ulitolewa na wagombea wawili wa nafasi ya urais wa Zanzibar, Juma Ali Khatib (Tadea) na Soud Said Soud, walipokuwa wakizungumzia kauli ya Zitto kudai haikuwa sahihi kwa Rais wa Zanzibar kubakia madarakani wakati serikali yake imefikia ukomo wake Novemba 2, mwaka huu. Soud alisema kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar Kifungu cha 28 (1)(a), Rais Shein ni Rais halali wa Zanzibar na atabakia madarakani hadi atakapochaguliwa rais mpya kwenye uchaguzi wa marudio. Alisema kuwa Dk. Shein alichaguliwa na wananchi wa Zanzibar na haikuwa haki kwa Zitto kumhusisha na makosa ya uhaini kwa kuendelea kubaki madarakani kwani yuko kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. "Zitto Kabwe afute kauli yake na kuwaomba radhi wananchi wa Zanzibar ndani ya siku 14 na

BREAKING NEWS : RAIS MAGUFULI AMSIMAISHA KAZI KAMISHA MKUU WA TRA

Picha
Aliyekuwa Kamishna wa TRA Rished Bade Rais John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi kamishna wa mamlaka ya mapato TRA Bw.Rished Bade na kumteua Bw.Philiph Mpango kukaimu nafasi hiyo. Taarifa kutoka ikulu zimesema kuwa uamuzi huo wa rais Magufuli umefuatia ziara ya waziri mkuu bandarini uliobaini upotevu wa makontena 349. Aidha rais Magufuli amemtaka Rished Bade kutoa ushirikiano kwa Philiph Mpango wakati uchunguzi ukiendelea.

BREAKING NEWS : WAZIRI MKUU AIBUA MADUDU YA UPOTEVU WA MAKOTENA 346 YENYE DHAMANI YA BILIONI 80

Picha
Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na uongozi wa TRA na TPA alipofanya ziara ya kustukiza Bandarini leo asubuhi. Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta madudu ambayo hakuyafurahia. Maafisa hao, ambao kwa sasa tunahifadhi majina ili Jeshi la Polisi liweze kuwashughulikia, wametakiwa pia kusalimisha hati zao za usafiri. Hii imekuja baada ya kugundulika kwamba kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani. Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiongea na viongozi wa TRA na TPA Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akikabidhi orodha ya makontena yaliyopotea na ambayo TRA haina taarifa nazo Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa akiagana na viongozi wa TRA na TPA.

Wizara Zinazotarajia Kufutwa na Magufuli Hadharani.......

Picha
Wakati kukiwa na taarifa kwamba Rais Dk. John Magufuli, anatarajia kupunguza karibu nusu ya wizara zilizokuwapo kwenye Serikali ya Awamu ya Nne, imefahamika kuwa wizara zinazolengwa ni zile zilizopo Ofisi ya Rais, Makamu wa Rais na Ofisi ya Waziri Mkuu. Chanzo kimoja kutoka serikalini kimeiambia Nipashe jana kuwa wizara hizo zitaunganishwa kwenye wizara mpya zitakazoanzishwa na Rais ambaye ameweka mkakati wa kuwa na baraza dogo la mawaziri. Wizara zinazotajwa kufyekwa ni Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Kazi Maalum, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu, Wizara Ofisi ya Waziri Mkuu na Sera, Uratibu na Bunge. Nyingine ni Wizara Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Wizara ya Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano, Wizara ya Nchi, Ofisi Makamu wa Rais Mazingira na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Kadhalika, katika mabadiliko hayo, wizar

Mtoto wa Alphonce Mawazo Akiwa na Lowasa Alipotoka Kufanya Mtihani wa Taifa Leo

Picha
Mtoto wa Kamanda wangu Alphonce Mawazo akiwa na Mhe Edward Lowasa alipotoka kufanya Mtihani wake wa Taifa wa darasa la Nne Tuko pamoja mtoto wa Rafiki yangu PreciousAlphonceMawazo  

PICHA ZA MISS TANZANIA AKIWA CHINA KWENYE MASHINDANO YA MISS WORLD

Picha
Safari ya  Miss Tanzania  kusogelea headlines za fainali za  Miss World 2015  imesogea hatua moja mbele ambapo mrembo wetu,  Lilian Deus Kamazima  tayari katua China kuungana na warembo wengine zaidi ya 100 toka nchi mbalimbali kushiriki kwenye fainali yenyewe. Kama hujajua basi naomba nikuweke karibu na ratiba yenyewe mtu wangu, ni kwamba Lilian aliondoka TZ  November 19 2015  kuelekea  Sanya China  ambapo watakaa kambi kwa muda wa kama wiki nne hivi. Fainali ya Miss World  itakuwa  December 19 2015  hukohuko  Sanya China , hapa nimezipata pichaz za warembo wote 20 wanaowakilisha nchi mbalimbali za Afrika kwenye fainali za  Miss World 2015. Lilian Kamazima , mwakilishi wetu  Tanzania  kwenye  Miss World 2015 . (Umri- 19) Mrembo kutoka Botswana , anaitwa  Seneo Bambino Mabangano  (Umri- 19) Anaitwa  Andrea N’Guessan Kakou , mrembo kutoka  Ivory Coast  (Umri- 23) Jina lake ni  Kisanet Teklehaimanot , mrembo kutoka  Ethiopia  (Umri- 21) Anaitwa  

BREAKING NEWS! UTURUKI YADUNGUA NDEGE YA URUSI!

Picha
Rais wa Urusi, Vladmir Putin, amesema kitendo cha Uturuki kuidungua ndege yake ya kivita mpakani mwa Syria, ni sawa na kuchomwa kisu mgongoni na kwamba ndege hiyo haikuwa na kitisho chochote kwa Uturuki. Rais wa Urusi, Vladmir Putin amesema kitendo cha Uturuki kuidungua ndege yake ya kivita mpakani mwa Syria, ni sawa na kuchomwa kisu mgongoni na kwamba ndege hiyo haikuwa na kitisho chochote kwa Uturuki. Akizungumza mjini Sochi, wakati wa mkutano wake na Mfalme Abdullah wa Pili wa Jordan, Putin amesema kitendo hicho kitakuwa na madhara makubwa katika uhusiano wa Urusi na Uturuki. Amesema watakitathmini kitendo hicho kubaini yale yote yaliyotokea. Amefafanua kuwa kitendo cha Uturuki kuidungua ndege yake ya kivita chapa SU-24, kimefanywa na washirika wa magaidi. Amekanusha taarifa kwamba ndege hiyo ambayo Uturuki inadai ilipuuza onyo walilolitoa, ilivuka mpaka wa Syria na kuingia katika anga ya Uturuki bila ya idhini, akisema imeangukia umbali wa kilomita 4

HAWA NDO WABUNGE 15 WAREMBO ZAIDI KATIKA BUNGE HILI JIPYA

Picha
Sifael Paul na  Brighton Masalu Upande wa pili! Bunge la 11 liliahirishwa Ijumaa iliyopita ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli aliwahutubia wabunge huku Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa akihitimisha hotuba kwa kuliahirisha rasmi bunge hilo hadi Januari 26, mwakani. Hata hivyo, hiyo siyo hoja wala gumzo kuu la bunge hilo ambalo linajumuisha wabunge wengi wapya kutoka vyama mbalimbali, lakini ‘pointi’ kubwa ni jinsi wabunge 15 wanawake ambao walilitikisa bunge hilo kutokana na urembo wao na kuzua gumzo kubwa. Wabunge hao warembo a.k.a visu ambao umri wao bado ni ‘asubuhi’, walikuwa kivutio machoni mwa baadhi ya wabunge hususan vijana ambao ‘walivunjika’ shingo juu ya wawakilishi hao. Ijumaa Wikienda  linakupa orodha ya wabunge hao warembo ambapo waliojulikana kwa kukimbiza kama akina Halima Mdee wametakiwa kukaa chonjo. Hata hivyo, wabunge warembo wa kike ni wengi, lakini wafuatao ndiyo ‘shida’ kuanzia maumbo na

EMIRATES WAIONJA JOTO YA JIWE FUMUA FUMUA YA RAIS DR. MAGUFULI SOMA HAPA HABARI KAMILI

Picha
Fumua fumua yamabadiliko ya Rais Dr. Magufuli hatimaye imewakumba Shirika la Ndege la Emirates ambalo sasa limepunguza safari zake za kuja Bongo kutokana na agizo la Magufuli la Maofisa wa Serikali kutosafiri nje ya bongo bila ya ruhusa maalum. Share kwa marafiki: TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

MANENO 34 YA MKE WA RAIS MUGABE WANAOVAA SKETI FUI NA SURUALI ZA KUBANA

Picha
Huu ujumbe umetoka kwa mke wa Rais wa Zimbabwe, Mama  Grace Mugabe  na umetolewa kwenda kwa warembo wote wanaopendelea vimini na suruali za kubana, anasema lolote baya likikukuta basi ujue umejitakia !! Kama na wewe uko kwenye list ya wanaopendelea kuvaa hivyo, basi maneno ya  Mama Mugabe  yakufikie >>> “ Kama unatembea huku umevaa kimini umeacha mapaja yako wazi, unawashawishi wanaume wakutamani.. hapo kama ikitokea umebakwa utalaumu? Huo ni ujinga wako mwenyewe .”– Mama  Grace Mugabe . Mama Grace Mugabe . Mama  Grace Mugabe  hakuishia hapo, ushauri wake ni huu hapa  “ Mnapaswa kuvaa kama mimi au kama unavaa suruali isiwe ya kukubana sana… “ Ujumbe wake unapingana na madai ya kikundi cha  Katswe Sisterhood , kilichopo  Harare Zimbabwe  ambao wamewahi kuandamana wakitaka wanawake kuruhusiwa kuwa na uhuru wa kujichagulia mavazi ya kuvaa

CHADEMA Washinda Kesi ya Pingamizi la Polisi, Sasa kesi ya Msingi kusikilizwa

Picha
Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Lameck Mlacha, ametupilia mbali mapingamizi yaliowekwa na RPC wa Mwanza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa mleta maombi ambae ni Baba mdogo wa Mawazo hana uhalali wa kisheria wa kuleta maombi hayo kwa kuwa yeye si baba mzazi wa marehemu, na kuwa hajaleta hoja za kubishaniwa kwenye maombi hayo. Upande wa utetezi unaoongozwa na mawakili John Mallya, James Millya na Paul Kipeja ulijibu hoja hizo kuwa katika hatua hiyo masuala ya kubishaniwa hayana sababu ya kuletwa kwa kuwa ni hatua ya awali sana. Kuhusu uhalali wa kisheria wa baba mdogo wa marehemu, majibu yalikuwa kwamba baba mdogo kwa kuwa ndiye aliemlea Marehemu Mawazo, anayo mamlaka na uhalali wa kisheria wa kuleta maombi hayo. Mahakama imekubaliana na hoja za mawakili wa mleta maombi na kuamua kuruhusu kesi ya msingi kufunguliwa kama ilivyoombwa, na kutupilia mbali mapingamizi ya RPC na AG. Upande wa wapeleka maombi utawasilisha maombi ya kesi ya msingi leo hii mch