RAIS DK MAGUFULI AKUSUDIA KUFUTA WIZARA HIZI 8


Siku chache baada ya kufuta safari za vigogo nje ya nchi,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Magufuli anakusudia kufyeka wizara 8 miongoni mwa 28 zilizopo sasa ili kubana matumizi.
Hatua hiyo ya Dr Magufuli ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwa wananchi wakati akijinadi kwenye kampeni zake za kuwania Urais kupitia Chama cha Mapinduzi-CCM kwamba atapunguza ukubwa wa serikali kwa kuunda baraza dogo la mawaziri.
Katika miaka 10 ya uongozi wa Rais Kikwete, kumekuwa na malalamiko ya ukubwa wa baraza la Mawaziri huku baadhi ya wizara zikiwa na mawaziri watatu.
Kwa mkakati huo,endapo Dr Magufuli ataweza kufyeka Wizara 8, maana yake atakuwa amewatupa nje ya ajira vigogo zaidi ya 20 ambao ni mawaziri na manaibu wao pamoja na makatibu wakuu na manaibu wao ambao kasma zao za mishahara ni mzigo mkubwa kwa serikali
Baraza la kwanza la Rais mstaafu Kikwete mwaka 2005 lilikuwa na Mawaziri na Manaibu wao 60, jambo ambalo lililalamikiwa na wadau wengi kwamba halina tija bali lilikuwa na lengo la kulipana fadhila
Taarifa zaidi zinasema kuwa huenda Rais Magufuli akachelewa uteuzi wa mawaziri hadi Disemba mwaka huu ili kujipa muda zaidi wa kuangalia na kufanya uchambuzi wa wizara zipi za kuzifyeka kwani baadhi hazina tija
Wizara zilizo Hatarini Kufyekwa
Ingawa Rais Magufuli hajazitaja Wizara zitakazofyekwa, lakini habari toka serikalini zinasema kuna uwezekano mkubwa wizara zisizo na tija na zinazoweza kuunganishwa na kuwa idara chini ya wizara fulani, zikafyekwa.
Wizara hizo ni Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto ambayo huenda ikaingizwa kwenye ofisi ya Makamu wa Rais, hasa wakati huu ambapo ofisi hiyo inashikiliwa na mwanamke.
Nyingine ni wizara iliyokuwa ikishughulika na mambo ya utawala bora ambayo wadadisi wa masuala ya siasa wanapendekeza iwe chini ya Wizara ya mambo ya ndani pamoja na Takukuru ili kukabiliana na Rushwa.
Wizara ya Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira nayo inaweza kufyekwa na suala la Mazingira likasimamiwa na kila Wizara kwa kuwa na kitengo chake cha kusimamia mazingira badala ya kuwa na Waziri wake.
Wizara ya uwekezaji na uwezeshaji huenda ikafutwa na kuingizwa ndani ya kituo cha uwekezaji ( TIC ) na kuwa idara nyeti ya kusimamia maswala ya uwekezaji ikiwa chini ya wizara ya Viwanda na Biashara.
Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo nayo inapumulia mashine kwani huenda ikaungana na Idara ya Habari (Maelezo) na kuwa idara zilizo chini ya ofisi ya Waziri mkuu badala ya kuwa Wizara kamili
Wizara ya Kilimo na Mifugo inapendekezwa kuwa moja badala ya mbili kama ilivyosasa.Waziri katika ofisi ya Rais (Kazi Maalumu) iliyokuwa inashikiliwa na Profesa Mwandosya yenyewe imekufa kifo cha Mende,kwani hakuna ubishi kwamba itafyekwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.