Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2014

SINEMA YA BURE LIVE: BABA WA MSANII ASHUSHA KICHAPO!

Picha
Baba huyo akizuiwa ili asiendelee kushusha kichapo hicho. Kwa mujibu wa mashuhuda wetu, tukio hilo lilijiri juzikati, maeneo ya Mwananyamala-Komakoma jijini Dar ambapo awali binti huyo ambaye ni msanii chipukizi wa kuigiza aitwaye Jeniffer alidaiwa kupigwa mkwara na baba yake kuwa asijishughulishe na masuala ya muvi na badala yake ajikite kwenye masomo yake kufuatia tasnia hiyo kuhusishwa na skendo za ngono.  Baba mmoja ambaye jina halikupatikana mara ameshusha kichapo kwa wasanii ambao ni maprodyuza waliokuwa wakimchezesha mwanaye filamu bila ridhaa yake

BREAKING NEWZZZ.........KAMATI YA BUNGE YATOA MAPENDEKEZO VIONGOZI HAWA WAFUKUZWE NA WASHTAKIWE...KUTOKANA NA KASHFA YA AKAUNTI YA ESCROW

Picha
PRO. MUHONGO MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI JAJI WEREMA MH.WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA PROF. ANNA TIBAIJUKA

Zitto: MAISHA YETU HATARINI!

Picha
Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC),Zitto Kabwe  Licha ya kumpongeza Mbatia na wenzake walioamua kufuatilia taarifa za kusambazwa na nyaraka hizo na kutoa taarifa, alisema anayehusika kuzisambaza ameshakamatwa na polisi, atashikiliwa mpaka atakaposema taarifa anazozisambaza amezitoa wapi.     Dodoma/Dar. Siku moja kabla ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuwasilisha bungeni, ripoti ya uchunguzi wa IPTL kuhusu ufisadi katika akaunti ya Escrow, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe amesema amekuwa akipata vitisho ili kuzuia ripoti hiyo. Akizungumza jana, Zitto alisema pamoja na vitisho hivyo haogopi kwa kuwa maisha yake ameshayaweka nadhiri siku nyingi. “Kuna kundi la wahuni kutoka Musoma limeletwa Dodoma likiongozwa na mtu (jina tunalihifadhi) mwenye rekodi ya ujambazi. Hivi sasa anashikiliwa na polisi kwa kukutwa na nyaraka zilizoibwa Ofisi ya Bunge. Usalama wa wajumbe wote wa PAC upo shakani,” alisema Zitto. Al

SHUHUDIA AJALI YA TOYOTA HAICE ILIYOUWA WATU TISA NA KUJERUHI WENGINE TISA SHINYANGA

Picha
Toyota haice yenye namba za usajili T761 CKD iliyokuwa ikitoka wilayani Kahama kuelekea mjni Shinyanga ikiwa imepinduka katika eneo la Buhangija manispaa ya Shinyanga na kuuwa watu tisa na kujeruhi wengine tisa,baada ya kupinduka mara tatu baada ya kuvuka tuta kisha kugonga daraja na kuangukia mtaroni,chanzo chake ni mwendo kasi ambapo dereva wa gari hilo Anwar Awadhi mkazi wa Lubaga Shinyanga aliruka na kukimbia.

CHAMELEONE:DIAMOND NIMSANII MCHANGA SIWEZI KUMUOMBA COLLABO

Picha
Chameleone amesema kuwa application ya Mziiki ambayo Diamond ni balozi wake wa Tanzania ipo kwenye mazungumzo naye ili kumfanya balozi wake wa Uganda na hivyo ilimuomba afanye wimbo na Diamond kama anthem ya Afrika Mashariki. “Lakini we talked about business na hatujamalizana nao. Lakini sio eti mimi nimempigia (Diamond) kumuomba tufanye collabo na kitu kama hicho,” amesema Chameleone. “Wale wa Mziiki app ndo wanahitaji mimi na yeye tufanye kazi ya anthem ya Mziiki app. Wanajaribu kuunganisha yeye na mimi tufanye collaboration lakini sio eti mimi nimemu whatsapp na nimemuomba collaboration , that’s not right,” amesisitiza hitmaker huyo wa Valu Valu. “Am not at a level of asking for a collaboration from any artist in that manner. Sio kwamba sina heshima yake (Diamond) au kitu kama hicho lakini that’s not the truth, haiwezi kuwa hivyo. I have been doing music for the past 14 years, right? So I am not an upcoming artist.”

MAMA SALMA KIKWETE AFUNGUKA JINSI ALIVYOKUTANA NA RAIS KIKWETE

Picha
Mama Salma kikwete MAMA SALMA  ;  Swali: Ni ipi historia fupi ya maisha yako? Jibu:  Mimi naitwa Salma Rashid. Nilizaliwa katika wilaya ya Lindi Mjini, Novemba 30, 1963. Baba yangu anaitwa Rashid Yussuf Mkwachu na mama yangu ni Mwanapaza binti Shariff. Kwa asili, baba yangu anatoka Sarai, Rufiji mkoani Pwani na mama yangu anatoka Lindi.

HII NDIO NYUMBA YA MSANII LADY JAYDEE KWA NDANI INAVYOONEKANA

Picha

MOMBASA HALI NI TETE,MSAKO WA POLISI MISIKITINI VIJANA WANNE WAFARIKI

Picha
  KIJANA alipigwa risasi na kuuawa na wenzake zaidi ya 250 kukamatwa kwenye operesheni kali ya kusaka magaidi mjini Mombasa jana.   BAADHI ya vijana waliokamatwa ndani ya misikiti ya Musa na Sakina, eneo la Majengo, Mombasa, wakati wa msako wa polisi usiku wa kuamkia jana ambapo kijana aliuawa na washukiwa zaidi ya 251 kukamatwa.Silaha mbalimbali zikiwemo gruneti, bastola, visu na mapanga zilipatikana ndani ya misikiti hiyo. Picha/LABAN WALLOGA Akihutubia wanahabari katika kituo cha polisi cha Urban, mjini Mombasa, afisa mkuu wa polisi (OCPD) Mahmoud Salim, alisema kijana aliyeuawa alijaribu kushamulia maafisa wa usalama kwa gruneti walipokuwa wakiingia msikitini.   “Walimpiga risasi kabla ya hajatupa gruneti hiyo na kumwua papo hapo,” akasema Bw Salim na kuapa kuwa operesheni hiyo itaendelea hadi wahalifu wote wanaswe.

MWANAMKE ALIYEJINGUNDULIA DAWA YA MICHEPUKO

Picha
Msichana aliyetajwa kwa jina la Abbie Bartlett, wa Ibiza Hispania, amewashangaza wengi baada ya kumvalisha mpenzi wake Leon Connolly fulana maalum yenye ujumbe unaowaponda wasichana wengine na kumsifia yeye kwa lengo la kujihami na wezi wa penzi lao. Abbie alifanya hivyo baada ya kuona kuwa mpenzi wake anataka kusafiri na kwamba wangekuwa mbali kwa muda mrefu hivyo alitaka maandishi pekee yawe ujumbe wa kutosha. Nampenda mpenzi wangu Abbie, nawachukia wasichana wa Ibiza, kwa hiyo tafadhali kaa mbali na mimi. Yanaeleza maandishi yaliyo kwenye fulana hiyo ikiwa na picha zao

Miss Tanzania Mpya 2014 Lilian Kamazima Yadaiwa Ni Mnyarwanda, Apondwa Kuwa Ni Mbaya.

Picha
Lilian Kamazima Mwenzako akinyolewa wewe tia maji !......Zengwe jipya limeibuliwa jana na kuenezwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Lilian Kamazima aliyepewa taji hilo baada ya Sitti Mtemvu ambaye ni mshindi wa awali kujivua taji kutokana tuhuma za kudanganya umri, si raia wa Tanzania bali ni Mnyarwanda. Hashim Lundenga ambaye ni Mkurugenzu wa Miss Tanzania, amekanusha vilivyo na kusisitiza kuwa ni uzushi kwa sababu wao wanaangalia vyeti vya kuzaliwa ambavyo vinaonyesha uraia wa mshiriki. Hayo yameibuka siku mbili tangu Lilian kukabidhiwa taji la Miss Tanzania 2014, lililokuwa likishikiliwa na Sitti Mtemvu aliyeamua kulivua baada ya kukumbwa na kashfa mbalimbali tangu kutawazwa kwake Oktoba 11. Ukiachilia mbali hilo la uraia tangu apewe taji hilo juzi kwenye mitandao ya kijamii mashabiki wa urembo wamekuwa wakimponda Lilian kuwa ni mbaya sio mzuri wa kuwa Miss Tanzania. Lilian ambaye awali alikamata nafasi ya pili kwa mujib

GADNER AMKANA LADY JAY DEE MCHANA KWEUPE...!! HII SI SALAMA.

Picha
7:58 PM     No comments Hii imetokea jana katika tamasha maalum la kituo kipya cha kazi cha Gardner E.FM ambapo Gardner alipanda jukwaani kujitambulisha mashabiki waliokuwepo wakamuuliza shemeji  Jaydee yuko wapi? Akawajibu i am single boy now kisha akaomba awekewe nyimbo ya Single boy ya Ali Kiba na kuicheza jukwaani huku akimpandisha jukwaani shabiki wa kike na kumwambia amvue tishet yake kimahaba kuthibitisha usingo boy wake ambapo demu huyo alimvua kwa staili hiyo gardner huku ukumbi ukilipuka kwa shangwe.

HATIMAYE VENGU APONA...APEWA NYUMBA YA MIL 120 ARUDI KWENYE LUNINGA

Picha
  Stori: Mwandishi Wetu MUNGU mkubwa! Vengu is back from hell (Vengu amerudi toka kuzimu). Msanii staa wa Kundi la Orijino Komedi ‘OK’, Joseph Shamba ’Vengu’ ameanza kurejea katika ‘fomu’ baada ya kuugua kwa muda mrefu, Risasi Jumatano linathibitisha.   Msanii staa wa Kundi la Orijino Komedi ‘OK’, Joseph Shamba ’Vengu’. Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa msanii huyo (jina tunalo), Vengu ambaye kwa muda mrefu alipoteza kumbukumbu kiasi cha kushindwa kuwatambua watu, sasa amejaliwa kwani anaweza kuwafahamu watu mbalimbali wanaopata nafasi ya kwenda kumjulia hali, Kigamboni jijini Dar anakoishi. AMEANZA KUTOA ‘HI’ KWA WATU “Bado yupo chini ya uangalizi maalum wa kifamilia, ni watu wachache wanaruhusiwa kumuona, lakini sasa hivi huwezi kuamini, watu wanaofika kumtazama anawatambua na anawapa ‘hi’. TATIZO USIRI Kutokana na usiri wa hali ya msanii huyo unaofanywa na familia yake, kumekuwa na maneno chini kwa chini ikiwa ni pamoja na uzushi wa mara

MISS TANZANIA "SITTI MTEMVU" ATOWEKA....

Picha
  suala la kudaiwa kudanganya umri likiwa bado ‘bichii’, taarifa zinadai kuwa mshindi wa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu ametoweka na hajulikani alipo, Risasi Mchanganyiko limechimbua stori kamili.   Mshindi wa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu. Shughuli ya kumsaka mrembo huyo ili kujua undani wa sakata lake ilianzia Temeke ambako ilielezwa kuwa ndiko anakoishi. Mapaparazi wetu walipofika katika nyumba waliyoelekezwa, walikuta imebadilishwa na kuwa Ofisi ya Vikoba ambapo mmoja wa wahudumu wa ofisi hiyo kwa sharti la kutoanika jina lake gazetini, aliwataka waandishi wetu kwenda Mbezi-Makonde akidai ndiko anakoishi kwa sasa. “Hapa ilikuwa nyumba ya zamani lakini kwa sasa ni ofisi na Sitti hakai hapa, kama mnamtaka nendeni Mbezi-Makonde huko nasikia ndiko anakoishi,” alisema mtumishi huyo. Mapaparazi wetu hawakuchoka, walifunga safari hadi Mbezi-Makonde ambapo walikut

RITA: MADUDU YA KINA SITTI MKIENDELEA KUYAFUMBIA MACHO TUTEGEMEE AIBU ZAIDI! KWENU

Picha
Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), bila shaka mko vizuri mnaendelea kusimamia jukumu zito katika taifa letu.Usajili, Ufilisi na Udhamini siyo kazi ndogo. Ni kazi inayohitaji umakini wa hali ya juu maana matokeo ya ufanisi wenu ndiyo majibu ya shughuli nyingi katika nchi. Watu wakitaka kusafiri, kutambulika katika maeneo mbalimbali nyinyi lazima mhusike kutatua. Mkitaka kujua afya yangu, mimi ni mzima. Namshukuru Mungu naendelea na majukumu yangu kama kawaida.  Nimewakumbuka leo kupitia barua hii ili niweze kuwafikishia yaliyoko katika akili yangu ndogo. Madhumuni ya barua hii kwanza kabisa ni kutaka… Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), bila shaka mko vizuri mnaendelea kusimamia jukumu zito katika taifa letu.Usajili, Ufilisi na Udhamini siyo kazi ndogo. Ni kazi inayohitaji umakini wa hali ya juu ma

NISHER AFUNGUKA KUHUSU SKENDO YA KUTEMBEA NA LULU, HIKI NDO ALICHOKISEMA…

Picha
Nisher ni kati ya watengenezaji bora wa video Bongo ambao wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuleta mabadiliko katika sekta hiyo. Jamaa huyu makazi yake yapo Arusha na kazi zake zote anafanyia huko. Kama ukiangalia video ya Jikubali iliyoimbwa na Ben Pol kisha Mama Yeyoo ya G.Nako ama video ya Nje ya Box au Chuna Buzi ya Shilole utatambua uwezo wake wa kuzipika video kiufundi. Juzikati Nisher alitinga ndani ya Global Publishers na kufanyiwa mahojiano katika Kipindi cha Mtu Kati kinachorushwa kupitia Mtandao wa Global TV Online na katika makala haya anafunguka zaidi: Unazungumziaje wasanii kurekodi video nje ya nchi?  Ni sawa kwani ni biashara na ni fedha ya mtu na huwezi kumkataza mtu anapotaka kuwekeza. Lakini kwa sanaa ya nchi yetu inatakiwa uangalie unatangaza vipi nchi yako. Muunganiko ni muhimu lakini usifanye muunganiko utakaokufanya ukawasahau madairekta wa nchi yako. Ni kweli tatizo ni mandhari ndiyo maana wanakimbia Bongo?  Hapana! Ujue mandhari hapa Bong

MAAJABU HARUSI YA NYANI INDIA YATIA FORA

Picha
Zaidi ya wakazi 200 katika kijiji kimoja kaskazini mwa India wamehudhuria sherehe ya harusi ya nyani wawili.  Harusi hiyo iliandaliwa na mmiliki wa nyani hao, ambaye alisema nyani dume ni kama "mwanaye". Sherehe hiyo ilifanyika siku ya Jumatatu katika wilaya ya Bettiah, katika jimbo la Bihar, huku "bi harusi" akiwa amevalia gauni maridadi.  Nyani ni viumbe wanaopendwa na watu wa jamii ya wa-Hindu. "Bwana harusi" ambaye anajulikana kama Ramu pamoja na mkewe mpya aitwaye Ramdulari walipitishwa katika mitaa ya kijiji wakiwa juu ya gari lililopambwa kwa maua na muziki ukichezwa, huku mamia ya wanakijiji wakijipanga kuwashangilia. Mmiliki wa nyani hao Udesh Mahto ambaye ana watoto watatu wa kiume amesema nyani Ramu ni kama mtoto wake wa kwanza. "Nilitaka yeye ndio aanze kuoa," ameiambia Idhaa ya BBC ya Kihindi. Bwana Mahto alimnunua Ramu kutoka Nepal miaka saba iliyopita, na baadaye kumnunua Ramdulari katika soko la kijiji.

WALICHOKISEMA MAPROFESA WA UDSM KUHUSU ISHU YA DIAMOND KUPEWA SHAHADA YA UDAKTARI

Picha
Ni kama wiki moja sasa tangu kuenea kwa habari ya kua Diamond Platnumz atapewa shahada ya Udaktari katika chuo kikuu cha Mlimani. Baada ya taarifa hizo kuenea sana tumebahatika kupata mahojiano ya maprofesa wawili kutoka chuo cha Mlimani wakizungumzia ishu hii. Wote wawili wamekubali kua Diamond ni msanii mkubwa lakini hajafikia hadhi ya kupewa shahada ya heshima ya udaktari.Angepata tu endapo tu angefanya jambo ubwa na kusaidia jamii na kwamba kuimba na kupendwa na watu si kigezo kikubwa cha kupewa tuzo hizo.

CHEKI VURUGU YA JANA KUMNUSURU WARIOBA!

Picha
  Kabla ya Jaji Warioba kuanza kuzungumza katika mdahalo huo ambao pia ulihudhuriwa na makada wa CCM na Chadema, Butiku alisema: “Hayawi hawayi, sasa yamekuwa. Tume imeshamiliza kazi na Bunge nalo lmeshamaliza kazi yake. Lengo ni moja tu, ni maendeleo yetu sote.” in Share Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa zamani, Jaji Joseph Sinde Warioba jana alivamiwa na kikundi cha watu wachache waliohudhuria mdahalo wa Katiba wakati akihoji vitendo vya baadhi ya watu kutumia vibaya jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.Jaji Warioba, ambaye alikuwa msemaji mkuu kwenye mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere, alikuwa akihitimisha hotuba yake aliyoianza saa 9:15 alasiri, kwa kuhoji kuhusu watu wanaotumia vibaya jina la Mwalimu Nyerere kupitisha hoja zao katika misingi isiyokubalika.Vurugu hizo zilidumu kwa takriban dakika

SITTI MTEMVU, MASAA, SIKU ZINAHESABIKA KUVULIWA TAJI LAKE BILA YEYE MWENYEWE KUPENDA

Picha
WAKATI serikali kupita Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), ikisema itakifuta cheti cha kuzaliwa cha Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu,  taarifa zinasema kwamba hawezi tena kuendelea na taji hilo. Imethibitisha kwamba uamuzi umekwisha kufanyika wa kumvua Sitti taji hilo alilovikwa katika mazingira tata, uamuzi unaotarajiwa kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa. Hata hivyo, haijafahamika kama hatua hiyo itachukuliwa na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) ama Sitti mwenyewe baada ya kubainika kwamba taji hilo linazidi kuiweka pabaya familia ya Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, ambaye ni baba yake. Imebainika kwamba hata hatua ya awali ya kuwania taji hilo ilichukuliwa na Sitti na baadhi ya wanafamilia bila kushirikishwa kwa Mbunge Mtemvu, jambo ambalo lilimsononesha awali katika ushiriki wa Miss Temeke. Imefahamishwa kwamba Mbunge Mtemvu amekerwa na hali inayoendelea ikiwa ni pamoja na kuwapo utata wa cheti cha kuzaliwa cha mwanae Sit

022014 Msanii KCEE wa Nigeria anunua Cadillac Escalade 2014 yenye bodi ya dhahabu (Gold Plated)

Picha
Gari hiyo imewekewa dhahabu na kampuni ya Malivelihood Luxury Designs. Hitmaker wa Pull Over, KCEE wa Nigeria ameonesha jeuri ya fedha kwa kununua gari aina ya Cadillac Escalade 2014 yenye bodi ya dhahabu. “So far this year God has been so good to me,sold out concerts,successful tours,endorsements e.t.c. So I decided to bless myself with a new Cadillac Escalade.

VURUGU: NGUMI ZAPIGWA WAKATI WA MDAHALO WA KATIBA

Picha
Jaji Warioba. VURUGU zilizoambatana na ngumi kurushwa zimetokea hivi punde katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam wakati aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba alipokuwa akitoa mada kwenye mdahalo wa kujadili umuhimu wa kuielewa kwa kina Katiba inayopendekezwa kama ilivyopitishwa na Bunge Maalum la Katiba. Vurugu hizo zimezuka baada ya watu waliokuwa na mabango kuvamia ukumbuni hapo na kusababisha baadhi ya watu… Jaji Warioba. VURUGU zilizoambatana na ngumi kurushwa zimetokea hivi punde katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam wakati aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba alipokuwa akitoa mada kwenye mdahalo wa kujadili