Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2019

Kusitishwa vikao vya bunge Uingereza kwazua hasira kali

Uamuzi wa waziri mkuu kusitisha bunge umesababisha ghadhabu kutoka kwa wabunge na wapinzani wanaopinga kuidhinishwa Brexit bila mpangilio. Hatua hiyo ilichangia kuzuka maandamano kote nchini, kesi iliowasilishwa dhidi ya hatua hiyo na waraka uliosainiwa na zaidi ya watu milioni moja kupinga hatua hiyo. Serikali imesema kuistishwa kwa wiki tano kwa vikao vya bunge mwezi Septemba na Oktoba kutaruhusu muda wa kutosha kujadili Brexit. lakini wakosoaji wanasema ni hatua "isio ya kidemokrasi " kuwazuia wabunge kupinga brexit bila ya mpangilio. Waziri Michael Gove ameiambia BBC kwamba kusitishwa huko kwa bunge kulikoidhinishwa na Malkia siku ya Jumatano 'bila shaka sio' hatua ya kisiasa kuzuia upinzani kwa hatua ya Uingereza kujitoa katika Muungano wa Ulaya pasi kuwepo mpangilio. Ameeleza kwamba kutakuwa na "muda mwingi" kujadili Brexit kabla ya muda ulioorodheshwa wa kuondoka Oktoba 31. Hapo jana Jumatano Bwana Johnson alisema hotuba ya

Ujerumani: Unyanyasaji waliofanyiwa wasichana wadogo enzi za Hitler

Unaweza kufikiria namna ambavyo kila sahani ya chakula chako inaweza kuwa ndio sahani ya mwisho kula. Mlo wako wa kifungua kinywa, chakula cha mchana na usiku pia vyaweza kumaliza maisha yako. Na lazima vyakula hivyo uvile hata kama unajua hatari iliyopo mbele yako. Kwa kundi la wanawake hukoThird Reich, maisha yao ya kila siku yalikuwa ni kuonja chakula cha Hitler kwa miaka miwili na nusu wakati wa vita ya pili ya dunia. Wanawake wadogo nchini Ujerumani walitakiwa kuonja chakula ambacho kilikuwa kimeandaliwa kwa ajili ya kiongozi huyo ili kubaini kama washirika wa Hitler walikuwa wanataka kumuwekea sumu. Kupata jukumu hilo ilikuwa ni heshima kubwa . Simulizi hiyo ya kushangaza juu ya wasichana ambao walikuwa na jukumu la kuonja chakula cha Hitler ilibainika mwaka 2013, kipindi ambacho mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 95, anayefahamika kama Margot Wölk alipobainisha kazi aliyokuwa anafanya zamani. Na sasa kuna mchezo wa kuigiza wa waonjaji wa chakula cha

Magufuli awataka Mabalozi kuleta miradi ya maendeleo nchini

Picha
Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ambayo inajengwa kwa fedha za Watanzania. Mabalozi hao 43 ambao wapo hapa nchini tangu tarehe 13 Agosti, 2019 wametoa pongezi hizo leo tarehe 22 Agosti, 2019 walipokutana na kuzungumza na Mhe. Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam. Wametoa pongezi hizo baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa bwawa la Nyerere litakalozalisha megawati 2,115 katika mto Rufiji, mradi wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (standard gauge railway) unaoanzia Dar es Salaam hadi Dodoma, jengo la 3 la abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam Jijini Dar es Salaam, mradi wa ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya barabara ya Morogoro na Sam Nujoma (Ubungo Interchange), mradi wa upanuzi wa bandari ya Dar es Salaam, mradi wa usambazaji wa gesi (Taifa Gas), mradi

Sudan: Abdalla Hamdok ateuliwa kuwa Waziri Mkuu

Picha
Sambaza habari hii Facebook   Sambaza habari hii Messenger   Sambaza habari hii Twitter   Sambaza habari hii Emai Haki miliki ya picha EPA Image caption Abdalla Hamdok alikuwa anafanya kazi Umoja wa mataifa Sudan imemteua Waziri Mkuu mpya ikiwa nchi hiyo ikiwa kwenye utawala wa mpito wa miaka mitatu chini ya uongozi wa jeshi . Waziri Mkuu Abdalla Hamdok anasema kuwa kipaumbele chake ni upatikanaji wa amani na kutatua changamoto ya kiuchumi . Uteuzi wake umekuja wakati ambapo Luteni Abdel Fattah Abdelrahman Burhan alichaguliwa kuwa kiongozi mpya wa baraza huru. Serikali mpya itaongoza taifa hilo mpaka kipindi cha uchaguzi. Kumekuwa na vurugu kwa miezi kadhaa ambayo imesababisha vifo vya waandamani wengi. Mwafaka wa kugawana mamlaka Sudan Mamluki katili wanaotawala nchi kwa dhahabu Omar el Bashir 'amepewa mamilioni kutoka Saudia' Upande wa upinzani una matumaini kuwa uteuzi mpya utaweza kusaidia kumaliza utawala wa kijeshi. Migogoro nchin

Je mwanamke mjamzito mwenye virusi vya ukimwi anaweza kumnyonyesha mwanae?

Je mwanamke mjamzito mwenye virusi vya ukimwi anaweza kumnyonyesha mwanae? Virusi vya HIV vinaweza kuingia kwenye maziwa ya mama na hivyo kumuambukiza mtoto wake wakati anapomnyonyesha Maambukizi ya virusi vya Ukimwi(HIV) imekuwa ni changamoto kwa akina mama walioambukia maradhi hayo wanaotaka kuwanyonyesha watoto wao mara baada ya kujigungua. Hii inatokana na hatari ya uwezekano wa mama kumuambukiza mwanae wakati anapomnyonyesha. Hofu hii hutokana kuongezeka kwa virusi vya HIV katika seli nyeupe za damu katika na maziwa ya mama anapokuwa mjamzito, hali inayoongeza uwezekano wa kumuambukiza mtoto wake virusi hivyo anapomnyonyesha. Viwango vya juu vya virusi katika plasma, na huenda katika maziwa ya mama, huonekana kama chanzo kikuu cha maambukizi ya virusi vya HIV kutoka kwa mama hadi mtoto na maambukizi hayo yamekadiriwa kuwa ni karibu 30%. Katika taifa la Rwanda akinamama walioambukia virusi vya ukimwi wanaweza kujifungua na kunyonyesha watoto wao bila kuwaambukiza mtoto.