Ujerumani: Unyanyasaji waliofanyiwa wasichana wadogo enzi za Hitler


Unaweza kufikiria namna ambavyo kila sahani ya chakula chako inaweza kuwa ndio sahani ya mwisho kula.
Mlo wako wa kifungua kinywa, chakula cha mchana na usiku pia vyaweza kumaliza maisha yako. Na lazima vyakula hivyo uvile hata kama unajua hatari iliyopo mbele yako.
Kwa kundi la wanawake hukoThird Reich, maisha yao ya kila siku yalikuwa ni kuonja chakula cha Hitler kwa miaka miwili na nusu wakati wa vita ya pili ya dunia.
Wanawake wadogo nchini Ujerumani walitakiwa kuonja chakula ambacho kilikuwa kimeandaliwa kwa ajili ya kiongozi huyo ili kubaini kama washirika wa Hitler walikuwa wanataka kumuwekea sumu.
Kupata jukumu hilo ilikuwa ni heshima kubwa.
Simulizi hiyo ya kushangaza juu ya wasichana ambao walikuwa na jukumu la kuonja chakula cha Hitler ilibainika mwaka 2013, kipindi ambacho mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 95, anayefahamika kama Margot Wölk alipobainisha kazi aliyokuwa anafanya zamani.
Na sasa kuna mchezo wa kuigiza wa waonjaji wa chakula cha Hitler, ulioandaliwa na Michelle Kholos Brooks ukiangazia hatari ambayo ilikuwa inawakabili katika maisha yao.
Ingawa mchezo huo umekuwa unapata vitisho kuonyeshwa Marekani lakini sasa mchezo huo utaweza kuonyeshwa katika tamasha kubwa la sanaa kidunia litakalofanyika mwezi mzima.
Wachezaji wote ni wanawake na imeangalia wasichana wenye umri kati ya miaka 15 ambao wako kwenye shule ambazo ziko karibu na makazi ya Hitler.
Mwandishi wa mchezo huo, Brooks alisikia kuhusu simulizi ya waonjaji chakula kwa bahati, mwandishi mwenzie alimwambia kuwa alisikia kuhusu hadithi hiyo pia wakati ambao walikuwa wanauliwa kabla hawajaondoka.
Alisema ," je nitaweza kuandika kuhusu hilo? kwa sababu kama sitaandika kuhusu hilo basi nitaenda kuandika" Brooks alikumbuka. Hadithi hii ilionekana moja kwa moja kuwa na maudhui mazuri.
Simulizi hii ilikuwa inagusa kila kitu ambacho nilikuwa ninakifikiria na kukihofa: namna ambavyo wanawake wadogo walivyokuwa wanatumikishwa, namna ambavyo watoto walikuwa wanaenda kwenye vita, kulikuwa na ugumu gani kwa wanawake na wanasiasa walikuwa wanawalaghai kwa namna gani..."
Sikutaka huo uhusika uwe kama historia, nilitaka kuangalia maisha ya sasa" - Michelle Kholos Brooks
Maigizo hayo ambao ni ucheshi umetengenezwa kumfanya mtu kutafakari historia na namna ambavyo wasichana wadogo walivyokuwa wakitumikishwa.
"Nilikuwa nikiwaangalia wasichana hawa wakiwa wanajipiga picha huku wakijituma kupata picha nzuri, na kutafakari kuwa hawa ndio wasichana haohao tofati ni nyakati tu. Hakuna utofauti zaidi ya muda tu" alisema Brooks alipokuwa anafafanua kuhusu mchezo huo, anasema alikuwa anawataka mabinti hao kuhisi kuwa ni wao na sio kwamba wanaigiza tu historia.
Mchezo huo uliweza kuelezea vita ya pili ya dunia kuifafanua kwa upana zaidi namna ambavyo wasichana waliokuwa wanakuwa walivyokuwa katika mazingira magumu.
Lakini vitu kuhusu maisha ya kuonja yalikuwa yanashangaza na jambo ambalo halikufaa kuwepo.
Ukilinganisha mfumo wa maisha ya watu wengi katika vita, walikwa wanaichukulia rahisi lakini mwaka 1944, watu wengi walikasirishwa sana na wajerumani
Ingawa wasichana hao walikuwa wanapata milo yote mitatu, chakula hicho kilikuwa akina nyama , kwa kuwa ndio chakula alichokuwa anakipenda Hitler na mwandishi alifafanua mlo kamili huo ulijumuisha wali, tambi na matunda kwa muda
"Licha ya kwamba chakula kilikuwa kizuri sana" aliongeza kuwa walikuwa hawafurahii chakula hicho
Chakula hicho ambacho kilikuwa ni mbogamboga kwa sababu Hitler alikuwa anakula nyama mara chache, wahudumu walikuwa wanaandaa chakula na kusubiri kwa saa moja kuangalia jinsi wasichana kama watadhurika au la, kama hawakudhurika basi chakula kilipelekwa kwa Hitler.
"Baadhi ya wasichana huanza kula chakula kwa wasiwasi na huku wakimwaga machozi," alisema mwanmke huyo aliyewahi kuwa muonjaji wa chakula cha Hitler wakati alipohojiwa mwaka 2013. "ilitupasa tule chakula na kusubiri saa moja , na mara zote hofu ya kuugua au kuona mwisho wa maisha yetu. Tulikuwa tunalia kama watoto wa mbwa pale tunapopona baada ya kula chakula hicho".
Katika kila chakula cha Hitler, wasichana hao wa kuonja chakula cha Hitler walikuwa wanategemea mawili baada ya saa moja kuisha kuwa ni kufa au kupona.
Mpaka sasa, hakuna wasichana ambao walidhurika na sumu ya chakula cha Hitler. Simulizi za mkasa wao haujasimuliwa sana na hata usingejulikana.
Ingawa inaonekana kuwa Wolk ndio muonjaji pekee wa Hitler ambaye alipona:
Inasemekana kuwa wasichana wengine waliuliwa na jeshi la Urusi kwa kupigwa risasi.
Aidha muonjaji chakula huyo wa Hitler amesifu namna ambavyo simulizi ya maisha yao imewezwa kusimulia kwa ucheshi "kutengenezwa kwa maigizo ya vichekesho katika hali ya namna hiyo ni njia nzuri ya uwasilishi" -mwanamke huyo alisifia.
na aliulizwa kama ni sawa watu kucheka katika mchezo huo au hata kukataa kuuangalia.
"Baadhi ya watu walisema kuwa hawataki kuangalia mchezo huo kwa sababu hawawezi kucheka kwa vitu viovu -lakini ukiangalia mchezo huo huwezi jua. "sisi hatumpendi Hitler" lakini mambo kama hayo yanabidi yasemwe.

Mchezo wa 'Hitler's Tasters' unahusu kucheka na wasichana hawa wadogo ambao walikuwa hawana hatia.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.