Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2019

Mchezaji wa Real Madrid Sergei Ramos amuoa Pilar Rubio

Harusi ya Sergio na Rubio iligubikwa na soka kwani nyota wengi wa soka walihudhuria Umati wa watu ulikusanyika katika kanisa kuu la Seville nchini Uhispania Jumamosi 15, Juni 2019, kushuhudia sherehe ya harusi ya mchezaji soka wa Real Madrid -Sergio Ramos aliyekuwa akifunga pingu za maisha na mchumba wake wa muda mrefu Pilar Rubio, ambaye ni mtangaza Televisheni. Sergio mwenye umri wa miaka 33-alikuwa nadhifu huku akiwa amevalia suti ya vipande vitatu nyeusi(three piece) iliyokuwa imeshonwa kwa mtindo wa aina yake pamoja na tai ya rangi ya kijivu iliyotulia huku bibi harusi mwenye umri wa miaka 41- akionekana kwa gauni lenye mvuto lililoiacha shingo na na mabega yake wazi kiasi cha haja. Haki miliki ya picha Getty Images Image caption Marco Asensio na mkewe Sandra Garal waling'ara kwa ajili ya harusi ya Sergio Ramos na Bi Pilar Rubio Gauni lake refu lililogusa sakafu lililikuwa limerembeshwa kwa shanga na juu alikamilisha urembo wake kwa shela iliyowekwa nakshi. Aliamua kus

Bajeti 2019: Tanzania na Uganda zapendekeza kodi kwa mawigi na visodo

Waziri wa fedha Tanzania' ametangaza kodi ya 25% kwa uingizaji wa nywele zote bandia maarufu mawigi na 10% kwa zinazotengenezwa nchini katika jitihada za kukuza uchumi wa nchi. Waziri Philip Mpango ametangaza hatua hizo, ambazo zitaidhinishwa mwanzoni mwa mwezi ujao kama sehemu ya bajeti iliyosomwa jana, ya mwaka 2019 na 2020. Kadhalika kodi kwa visodo imerudishwa kutokana na kwamba hatua ya kuondoshwa kodi mwaka jana kwa bidhaa hizo muhimu kwa wanawake, haikusaidia kushuka kwa bei. Na badala yake Mpango ameeleza kuwa ni wafanya biashara wanaofaidi kutokana na kuondolewa kwa kodi hiyo. wanawake wengi huvaa nywele hizo bandia ambazo kwa wingi husafirishwa kutoka mataifa ya nje . Kwa makadirio, wigi hugharimu kati ya $4 na hata zaidi ya $130. Kwa nini wanawake wanakuza nywele zao mwezi Januari Meya awasuka nywele wanawake kuvutia kura Ghana Je mtindo wako wa ususi unamaliza nywele zako kichwani? Nchi ya Uganda, pia imeidhinisha kodi kwa mawigi, ndevu bandia, kope na nyusi za kuba

Kenya: Mwanafunzi wa Chuo Kikuu akamatwa kwa kuingia Ikulu kinyume cha sheria

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) nchini Kenya, Brian Kibet Bera, anauguza majeraha katika katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta baada ya kupigwa risasi na polisi kwa kuingia Ikulu ya Nairobi kinyume cha sheria.Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye alikwea lango moja la Ikulu, alipigwa risasi na kujeruhiwa bega la kushoto na maafisa wa polisi wanaopiga doria kwenye lango hilo baada ya kuchomoa kisu alipoagizwa asimame.Siku ya Jumapili Jioni Kibet aliandika katika mtandao wake wa Facebook kuwa ataingia Ikulu. Tomorrow I attack State House. God has sent me to execute judgement on every thief and every partner of a thief,” - Kibet Bera pic.twitter.com/3qIzntofat — ktn (@KTNKenya) 11 Juni 2019 Kwa mujibu wa msemaji wa Ikulu, Kanze Dena-Mararo Kisa hicho kilitokea Jumatatu na mshukiwa alipelekwa katika Kituo cha Polisi cha Kileleshwa na kusajiliwa katika Kitabu cha Matukio nambari 39 kabla ya kupelekwa katika Hospitali ya Kitaifa ya

Uganda: Polisi Esther Naganda anayedaiwa kupigwa adai Shilingi milioni 200

Afisa wa polisi mwanamke wa Uganda anayedaiwa kushambuliwa na Meja Generali Matayo Kyaligonza na walinzi wake wawili amefika mahakamani kuomba apewe fidia ya shilingi za Uganda milioni 200. Mwezi Februari video inayodaiwa kuwa ni ya Afisa Namaganda akiburuzwa na kupigwa na watu wanaodaiwa kuwa walikuwa ni walizi wa Meja Generali Matayo Kyaligonza iliibua hisia kali kwenye mitandao ya kijamii nchini Uganda na nje ya nchi hiyo. Awali walinzi wa Meja Jenerali Kyaligonza walikamatwa kuhusiana na kisa hicho Akiwa Mahakamani Bi Esther Namaganda- ambaye ni Afisa wa usalama barabarani , anataka pia alipwe shilingi milioni 1 kama gharama ya uharibifu aliotendewa , Shilingi milioni 200 kama jenerali na adhabu kwa kosa alilotendewa la kuumizwa, kisaikolojia na kimwili na kusababishiwa aibu aliyopata wakati alipodaiwa kupigwa na mkuuu wake mwenye umri wa miaka 73-ambaye pia ni balozi wa Uganda nchini Burundi. Februari 24, 2019 Bi Namaganda alisema kuwa wakati alipokuwa kazini kwenye kituo c

Athari za pombe!

Jumla ya rekodi ya matumizi ya pombe kwa kila mwananchi (15 +), kwa lita za pombe halisi La muhimu zaidi katika madhara yanayoweza kutokea kufuatana matumizi ya muda mrefu ya ethanoli. Zaidi ya hayo, katika wanawake wajawazito,husababisha dalili za ulevi wa kijusi. Athari za matumizi mabaya ya pombeViwango vya juu vya matumizi ya pombe huhusiana na ongezeko la hatari ya kuendeleza ulevi, ugonjwa wa moyo, kutofyonza vyakula, ugonjwa sugu wa kongosho , ugonjwa wa ini kutokana na pombe, na kansa. Uharibifu kwa mfumo mkuu wa neva na mfumo wa neva za pembeni unaweza kusababishwa matumizi kila mara ya pombe. Matumizi ya pombe kupita kiasi kwa muda mrefu yanaweza kuharibu takribani kila kiungo na mfumo katika mwili. Ubongo unaokua wa kijana aliyebaleghe huwa hasa katika hatari kubwa ya kudhurika na sumu ya pombe.