Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2016

CUF Waitupia Lawama Serikali kwa Kushindwa Kuwajibika na Kuruhusu Uingizwaji wa Simu FEKI

Picha
Jumuiya ya Vijana CUF (JUVICUF) imeitaka Serikali kubeba mzigo wa kushindwa kuwajibika ipasavyo kwa kuruhusu uingizwaji wa simu feki nchini. Kauli ya jumuiya hiyo imekuja wakati imebaki mwezi mmoja kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuzima simu feki zote. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mtendaji wa JUVICUF, Mahamoud Mahinda Ally alisema Serikali ilishindwa kutimiza wajibu wake wa kuhakikisha simu hizo haziingizwi nchini, hivyo inapaswa kuwajibika. Ally alisema Serikali ilipaswa kuziba mianya hiyo tangu mwanzo na kwamba inachofanya sasa ni kukosa huruma kwa watu wake. Alisema kitendo cha wananchi kuachwa wakinunua simu feki siku za nyuma bila ya kudhibiti uingizwaji wake nchini ni kutozingatia matakwa ya haki za binadamu. “Kuruhusu simu feki ziingie nchini, kisha kuzizima ni mapambano ambayo Serikali inapambana dhidi ya wananchi wake,” alisema Ally. Akizungumzia kuhusu hilo, Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocen

Naibu Waziri Ajibu swali Lililomponza Kitwanga.....Asema Serikali Imekusudia Kujenga Nyumba 9500 Kwa Ajili Ya Askari Magereza

Picha
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Yusufu amejibu upya swali lililomponza bosi wake wa zamani, Charles Kitwanga. Uamuzi wa kurudia swali hilo ulitolewa juzi na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisema swali hilo lilijibiwa katika hali ya ulevi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na wabunge wakaomba mwongozo kuhusu majibu yaliyotolewa. Kitwanga aliondolewa katika nafasi yake na Rais John Magufuli baada ya kujibu ya swali hilo akiwa amelewa. Leo, Masauni amejibu swali hilo namba 211 la Mbunge wa Viti Maalumu Devota Minja (Chadema) na kuonyesha utofauti mkubwa kati ya majibu yake na yale yaliyotolewa mwishoni mwa wiki na aliyekuwa Waziri wake. Swali hilo ambalo awali lilikuwa namba 205, liliulizwa na Devota Minja akitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kuboresha makazi ya polisi na askari magereza wanaoishi katika nyumba chakavu zisizokuwa na hadhi ukilinganisha na kazi zao kwa jamii. Nyakati zote hizo, swali hilo limeulizwa na wabunge tofauti wa C

Chadema Wamtaka Rais Magufuli Amfuate Lowassa Ili Amshauri Kuhusu Sukari

Picha
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemtaka Rais John Magufuli kuweka siasa kando na kuomba ushauri kwa waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ili kutatua tatizo la kuadimika kwa sukari. Kauli hiyo ilitolewa na naibu katibu mkuu wa Chadema, Salim Mwalimu juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Moto wilayani Monduli Mkoa wa Arusha ambako Lowassa alizungumza na wananchi kuwashukuru kwa kumpigia kura na akatangaza mpango wa kuzunguka nchi nzima kwa lengo hilo. Tangu Rais atangaze kudhibiti uagizaji sukari kutoka nje na baadaye Bodi ya Sukari kutangaza bei elekezi, bidhaa hiyo muhimu imepanda bei kutoka Sh1,800 hadi kufikia Sh5,000 kwa kilo na kwa sasa imeadimika madukani, wakati Serikali ikisaka wafanyabiashara inaowatuhumu kuwa wa

BREAKING NEWZZ…..MKURUGENZI ALIYETUMBULIWA NA RAIS AFARIKI DUNIA ..NI STEVEN KEBWE

Picha
BREAKING NEWZZ…..MKURUGENZI ALIYETUMBULIWA NA RAIS AFARIKI DUNIA ..NI STEVEN KEBWE Inadaiwa amefariki dunia akiwa nchini India alikokuwa kwa matibabu. Aidha, inasemekana tangu siku ile wamtumbue jipu ktk Daraja la Kigamboni (Nyerere Bridge) alikuwa shocked sana alikuwa kalazwa India akipatiwa matibabu.

Lady Jaydee Kumuanika Mpenzi wake Ambae ni Mrithi wa Gardner Leo!

Picha
Exclusive! Lejendari wa Bongo Fleva kwa zaidi ya miaka kumi na tano, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee au Jide’, anatarajia kumuanika mrithi wa aliyekuwa mumewe, Mtangazaji wa Kituo cha Radio CloudsFM, Gardner G. Habash ndani ya saa 24, Ijumaa lina data kamili. HABARI ZA KUAMINIKA Kwa mujibu wa habari za kuaminika zilizothibitishwa na uongozi wa staa huyo, Jide atamtambulisha mchumba wake huyo kwa mara ya kwanza ndani ya Ukumbi wa Mlimani City leo, Dar ambapo pia atafanya shoo ya saa tatu mfululizo, inayokwenda kwa jina la Naamka Tena. “Itakuwa ‘sapraizi’ kwa mashabiki wote wa Jide ambapo sapraizi hii itaendana na shoo ya kihistoria ya Naamka Tena atakayoipiga kwa saa tatu akiwa na bendi yake (Lady Jaydee and The Band),” alisema mmoja wa viongozi wanaomsimamia ambaye hakutaka kutajwa gazetini. JIDE ALIPOTOKEA Jide alifunga ndoa na Gardner Mei 14, 2005 ambapo waliishi na kufanikiwa kuwa na mali mbalimbali ikiwemo ujenzi wa nyumba, Ukumbi wa Ny

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Katika Magazeti na Mitandaoni leo 19 May 2016

Picha
Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Katika Magazeti na Mitandaoni leo 19 May 2016 Job Opportunities at Access Bank Tanzania, Application Deadline 19 May 2016 Job Opportunities at Palladium Group, Application Deadline 27 May 201 6 Job Opportunity at Sanitation and Water Action, Application Deadline: 28 May 2016 Job Opportunities at Tanzania Postal Bank, Application Deadline: 27 May 2016 Job Opportunity at Las Vegas Casino, Application Deadline: 31 May 2016 Job Opportunity at Jhpiego, Application Deadline: 31 May 2016 Job Opportunity at RTI International,Application Deadline 24 May 2016 Au Tembelea  www.ajirayako.com  Kwa Kazi zaidi

Ndege ya Kivita ya Marekani Yaanguka na Kuungua na Moto Vibaya....

Picha
Ndege ya kivita ya Marekani aina ya B-52 imeanguka muda mfupi baada ya kupaa kutoka kwenye kambi ya taifa hilo eneo la Guam. Jeshi la Marekani limesema wanajeshi wote saba waliokuwa kwenye ndege hiyo walifanikiwa kuruka salama kutoka kabla ya ndege hiyo kuteketea. Ndege hiyo ilikuwa imepaa kutoka kituo cha jeshi cha Andersen. Picha zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zimeonesha moshi mkubwa ukitanda angani kutoka kwa vifusi vya ndege hiyo. Ndege hiyo, ambayo hutumiwa kuangusha mabomu, ilitumwa Guam kutoka jimbo la North Dakota na ni sehemu ya juhudi za Marekani za kuendeleza uwepo wake kijeshi katika bahari ya Pasifiki. Gavana wa jimbo la Guam amenukuliwa na tovuti ya habari ya Kuam akisema kwamba halikuwa shambulio. Ndege aina ya 5-52 zimetumiwa na Marekani kwa miaka 60 sasa, na zilichangia sana vita Vietnam na Afghanistan. Guam ni jimbo linalomilikiwa na Marekani eneo la Micronesia, Pasifiki magharibi na hupatikana kilomita 6,000 magharibi mwa Hawaii.

Machozi Band Imekufa Haipo Tena, Sitaki Kuitwa Binti Machozi Tena- LadyJaydee

Picha
Akongea na East Africa Tv Jaydee amsema ameamua kubadili jina hilo kwani hata yeye sasa hivi hatumii jina la Binti Machozi, akiamini msemo wa watu kuwa jina huzaa maana yake kwenye maisha. "Band kwa sasa haaitwi tena Machozi Band, inatwa The Band, nilibadilisha miaka miwili iliyopita na kwasababu sasa hivi mwenyewe sikutaka kuitwa binti machozi, watu wanasema jina unaloitwa linarelate na maisha yako, so nikaamua kubadili, kwa hiyo Machozi Band haipo tena imekufa, kwa sasa itakuwa ni lady jaydee and the band", alisema Jay dee. Jaydee ambaye mwisho wa wiki hii anayatajia kufanya tamasha kubwa la 'Naamka tena', amesema tamasha hilo litakuwa ni la masaa matatu bila kupumzika, kwani ana nyimbo zaidi ya 100 ambazo zinaweza zikamfanya afanye show zaidi ya masaa matatu.

Nani aligharamia ukarabati wa kifahari wa ofisi ya Mkuu wa mkoa

Picha
Picha zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao kuonyesha ufahari wa hali ya juu wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa dar es salaam. Ofisi hiyo imekuwa tofauti kabisa na ile ya Mkuu wa mkoa aliyepita bwana Sadick, ofisi ya Makonda ina kompyuta kadhaa za apple,mapambo mengi ya kila aina yanayoashiria ufahari na utukufu wa hali ya juu kuliko hata ofisi ya rais. Nani aligharamia ufahari huu wakati hata ikulu haijabadili muonekano? Kulikuwa na umuhimu wa kuweka ufahari huo katika kipindi hiki cha kubana matumizi? Nini kilipungua katika ofisi ya aliyekuwa Mkuu wa mkoa mpaka ufahari uongezwe katika jiji ambalo limezungukwa na wananchi wenye hali ngumu na maisha yasiyoridhisha. By iparamasa

Kutoielewa sheria ya makosa ya mtandao kutawaponza wengi

Picha
Tecno, Huawei na simu zingine za sqmartphone zenye bei chee zimewafanya watu wengi kuweza kufaidi ukuaji wa teknolojia. Lakini pia uwepo wa simu hizo, usingeweza kukamilika pasipo makampuni za mitandao ya simu hapa nchini kuboresha miundombinu ya internet. Kwa sasa kila mwananchi, hata wale wa vijijini wana access na internet. Hadi sasa kwa mujibu wa mamlaka ya mawasiliano nchini, TCRA zaidi ya watanzania milioni 17 wanatumia internet. Ndio maana kuna ongezeko kubwa la matumizi ya mitandao ya kijamii hususan Facebook, Instagram na WhatsApp. Ni WhatsApp kutokana na umuhimu wake imetokea kuwa mtandao unaotumiwa na wabongo wengi. Huko kuna makundi ambayo watu huchat, hutumiana video na picha kutaarifiana na mara nyingi kujifurahisha. Lakini pia ongezeko la matumizi ya simu, internet na mitandao ya kijamii imefanya kuwepo na matumizi mabaya na hivyo kupelekea kuanzishwa kwa sheria ya makosa ya mtandao. Lakini bahati mbaya ni kuwa pamoja na Watanzania wengi kujua

Vijana Wanaovaa Suruali Chini ya Kiuno Kuchapwa Viboko 70

Picha
Wakazi wa Kata ya Karansi, Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro wametoa uamuzi kuwa wanawake watakaovaa sketi fupi na vijana watakaovalia suruali chini ya kiuno, wataadhibiwa kwa kuchapwa viboko 60 hadi 70. Uamuzi huo umefikiwa na wakazi zaidi ya 200 wakisema uvaaji huo ni kinyume na mila na desturi za Kiafrika. Vazi lingine lisilotakiwa kwa wanawake ni kuvaa suruali pamoja na vijana kunyoa ndevu mitindo isiyofaa. Mkutano huo ulioandaliwa na wazee wa kimila jamii ya Meru (Wachili) na Wamasai (Malaigwani), uliwavutia wananchi wengi ambao walihudhuria. Sambamba na uamuzi huo utakaokuwa unafanyika hadharani, pia adhabu hiyo itawahusu wezi wa mali na wanaopenda kucheza pool table wakati wa kazi. Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Wilbrod Mutafungwa alipinga uamuzi huo akisema kwa maazimio hayo ya kuwaadhibu watuhumiwa kwa kuwachapa viboko ni kujichukulia sheria mkononi na ni kinyume na sheria.

RAIS MAGUFULI ATAJA MALI ZAKE AKASIRISHWA NA UDAGANYIFU AIRPORT

Picha
  Magufuli aliyeingia Ikulu Novemba 5, mwaka jana, alikuwa Mbunge ama waziri kwa miaka 20 mfululizo, akitumika kama Naibu Waziri wa Ujenzi na baadaye Waziri kamili kwenye Wizara mbalimbali. Kamishna wa Tume ya Maadili, Jaji mstaafu Salome Kaganda alilieleza Nipashe katika mahojiano maalum hivi karibuni kuwa Rais Magufuli alishawasilisha kwenye tume hiyo orodha ya mali alizonazo. Jaji Kaganda alisema Rais Magufuli aliwasilisha fomu inayoonyesha mali alizozipata kwa muda wote alipotumikia nyadhifa mbalimbali serikalini, kabla ya kuingia Ikulu. Nipashe lilizungumza na Jaji Kaganda kujua kama Rais Magufuli alishatoa tamko kama Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995 na kanuni zake zinazoeleza, lakini pia kufahamu idadi ya mali anazomiliki Rais huyo na thamani yake. Kaganda ali

Rais Magufuli Afanya Ziara ya Kushtukiza Uwanja wa Ndege..Akuta Madudu ya Hatari..Aagiza Hatua Kuchukuliwa

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuchukua hatua mara moja dhidi ya dosari za ukaguzi zilizopo katika kitengo cha ukaguzi wa mizigo na abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (Terminol One) Jijini Dares salaam. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 13 Mei, 2016 alipofanya ziara ya kushtukiza katika uwanja huo na kubaini kuwa mashine za ukaguzi za sehemu ya kuwasili abiria na mizigo hazifanyi kazi kwa muda mrefu. Maafisa wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere waliokuwa wakitoa maelezo juu ya hali ya kitengo cha ukaguzi wa mizigo na abiria katika uwanja huo, walikuwa wakitoa taarifa zinazo tofautiana kuhusu utendaji kazi wa mashine za ukaguzi, hali iliyosababisha Dkt. Magufuli kuamua kuiagiza wizara husika kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuchukua hatua mara moja. 'Unaju

Mwanamume 'Adandia' Helikopta Kenya

Picha
Mwanamume mmoja katika mji wa Bungoma, Magharibi mwa Kenya ameshangaza wengi baada ya kudandia helikopta ambayo imepaa na kuondoka naye. Helikopta hiyo ilikuwa imesafirisha mwili wa mfanyabiashara mashuhuri Jacob Juma aliyeuawa kwa kupigwa risasi jijini Nairobi wiki iliyopita, vyombo vya habari nchini Kenya vinasema. Video zinazosambaa mtandaoni zinaonesha helikopta hiyo ikipaa juu angani kutoka uwanja wa Posta, mwanamume huyo akiwa amejishikilia kwenye vyuma vya helikopta hiyo. Taarifa zinasema baadaye ndege imetua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Bungoma na mwanamume huyo akapelekwa hospitalini. Wengi wameeleza kushangazwa kwao na wengine wanalifanyia mzaha. Baadhi wanasema mwanamume huyo alisahau leo ilikuwa Ijumaa tarehe 13, ambayo kwa baadhi ni siku yenye kutokea mabaya.

Kibarua cha Rais wa Brazil Chaota Nyasi, Apigiwa Kura ya Kutokuwa na Imani Naye

Picha
Kitumbua cha Rais wa Brazil, Bi. Dilma Rousseff kimeingia mchanga. Baraza la senate limempigia kura ya kutokuwa na imani naye. Hiyo inamaanisha kuwa atakaa benchi na kupelekwa kortini. Bi Rousseff anatuhumiwa kulaghai hesabu za kifedha ili kuficha deni la umma linalokua kabla ya uchaguzi wa mwaka 2014, kitu anachokanusha. Maseneta walipiga kura 55 za kumuondoa katika mkutano uliodumu kwa zaidi ya saa 20. Ni 22 tu ndiyo waliokuwa upande wake. Makamu wa Rais, Michel Temer atakaimu nafasi yake wakati kesi ya Bi Rousseff ikianza kusikilizwa. Kesi hiyo inaweza kuchukua siku 180 hiyo inaamanisha kuwa atakuwa amesimamishwa katika kipindi ambacho michuano ya Olimpiki jijini Rio de Janeiro itaanza, August 5.

Siri za Matajiri Tanzania Kusajili Kampuni Nje ya Nchi

Picha
Wakati Mamlaka ya Mapato (TRA) ikijiapiza kuzifanyia uchunguzi wa kina kampuni za Kitanzania zilizoanzishwa nje ya nchi, wataalamu wameeleza jinsi wafanyabiashara wanavyotumia njia hiyo kukwepa au kuepuka kodi. Jana, mkurugenzi wa elimu ya mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo alisema ripoti ya Panama Papers ni chachu ya mamlaka hiyo kufanya uchunguzi wa kina na wa kimataifa ili kujua iwapo kuna chembechembe za ukwepaji kodi kwa kampuni hizo za Watanzania. “Kwa kutumia mbinu tulizonazo, tutafuatilia iwapo kampuni hizo zimekwepa kodi wanayopaswa kulipa hapa nchini,” alisema.  Kayombo alisema watatumia mbinu zote, kama Polisi wa Kimataifa(Interpol) na benki zinazohusika pamoja na kuchunguza miamala iliyofanywa na kampuni hizo kujua iwapo wamekwepa kodi. “Hatuwezi kuzungumza kwa kina kwa sababu tutaharibu uchunguzi wetu, lakini kwa kifupi tutawa-trace (wafuatilia) wote,” alisema.  Juzi, timu ya Umoja wa Waandishi wa Habari za Uchunguzi (ICIJ), yenye makao makuu Washi

PICHA:Waziri Mkuu Akiwasili Ukumbi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi London Kumwakilisha Magufuli

Picha
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiingia ukumbi wa Lancaster House, London kuhudhuria mkutano wa Wakuu wa Nchi kuhusu mapambano dhidi ya Ufisadi Waziri Mkuu ameshiriki katika Mazungumzo Rasmi ya Wakuu wa Nchi, akimwakilisha Rais Magufuli

Kwa hili la Kukataa Mwaliko wa Uingereza, Rais Sikuungi Mkono

Picha
Rais John Magufuli amepata heshima ya pekee kualikwa na waziri mkuu wa Uingereza katika mkutano utakaofanyika kuzungumzia mikakati ya mapambano ya rushwa ikiwa ni nchi mbili tu zimepata fursa hiyo kwa bara la Africa ikiwemo pia Nigeria. Lakini Rais wetu amedai sasahivi amebanwa na majukumu kwahiyo atawakilishwa na Waziri mkuu mh. Kassim Majaliwa

Kigwangalla Amtaka Gardner Aombe Radhi kwa Kumdhalilisha Lady Jaydee

Picha
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Hamis Kigwangalla, amemtaka mtangazaji wa Clouds FM, Gardner G Habash kumuomba radhi aliyekuwa mke wake, Lady Jaydee kwa ‘kile alichokiita’ kama udhalilishaji kwake na kwa wanawake wote. Wikiendi iliyoisha imesambaa video mtandaoni ikimuonesha mtangazaji huyo akiongea kwenye tamasha alilokuwa mshereheshaji: "My name is Captain Gardner G Habash all the way from Clouds FM, Jahazi hatari sana. Na sina neno na yule mtoto wa kike. Nimeshamkojoza kwa miaka kama 15 hivi.” Video hiyo imesababisha hasira kubwa kwa mashabiki wa Jaydee na watu wengi kwa ujumla. “Ndg. Gardner amefanya udhalilishaji mkubwa si tu Kwa @JideJaydee bali ametukana wanawake wote. Mimi #BaloziWaWanawake namtaka aombe radhi,” ameandika mheshimiwa Kigwangalla kwenye Twitter. “Natoa rai kwa uongozi wa @cloudsfm kumtaka Ndg. Gardner afute kauli yake na aombe radhi kwa @JideJaydee na kwa umma ili kulinda heshima yao,” ameongeza.

SUMATRA yatangaza nauli kwa mabasi yaendayo kasi

Picha
Baada ya Kampuni ya UDA-RT kuwasilisha maombi ya nauli zitakazotumika kwa mabasi yaendayo haraka kwa Mamlaka ya udhibiti usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA), leo hii (May 09 2016) SUMATRA imetangaza nauli hizo. SUMATRA imesema kuwa njia ya pembezoni (Freeder Route) nauli ya mtu mzima ni 400 na mwanafunzi 200 na njia kuu (Trunk Route) ni 650 na mwanafunzi 200 na kwa abiria atakayetumia kusafiri njia kuu (Freeder Route) na kuendelea na safari kwa njia ya pembezoni nauli yake itakuwa ni 800 na mwanafunzi 200. Huduma hiyo itatolewa kuanzia kesho bure kwa wananchi kwa siku mbili mfululizo na ifikiapo May 12 2016 zitaanza kutozwa nauli zilizotajwa. Msimamizi wa mradi kutoka DART, Injinia Ronald Lwakatare amesema haya wakati akiongea na waandishi wa habari mchana huu; ‘Wakati huo tunafanya majaribio tutakuwa tunaangalia mfumo unavyofanya kazi kwa hiyo tutawabeba abiria kwa siku kadhaa bila kulipa nauli’.

Bush Asema Hatampigia Kura Donald Trump

Picha
Aliyekuwa mgombea wa urais wa tiketi ya chama cha Republican nchini Marekani, Jeb Bush amesema hatampigia kura Donald Trump katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika nchini humo Novemba mwaka huu. Bush alisema kuwa Trump hana tabia wala mienendo ya kuwa Rais wa Marekani. ‘‘Marais wa Marekani wanasifa zao na wanakubalika kwa watu, lakini huyu jamaa hana sifa hata moja ndiyo maana kila siku namkana na kusema hafai kabisa kuwa rais wa nchi hii, ’’alisema Bush Jeb ni mojawapo wa wanachama mashuhuri wa Republican kutanganza hadharani kuwa hatampigia kura Trump kwa sababu ya kampeni yake ya kiburi ambayo imegawanya Chama cha Republican. Juzi Spika wa Bunge, Paul Ryan alisema hatamuunga mkono mfanyabiashara huyo tajiri ingawa atakutana naye wiki ijayo. Hata hivyo, Trump aliungwa mkono na mgombea urais wa zamani wa nchi hiyo, Bob Dole aliyeshindwa katika uchaguzi na Bill Clinton wa Chama cha Democratic mwaka 1996. Wiki iliyopita Seneta wa Texas, Ted Cruz alijitoa katika kin

Rais Mugabe Apigwa Kibao na Mkewe Hadharani...

Picha
Rais wa Zimbabwe Bw. Robert Mugabe amepigwa kibao hadharani na mkewe Grace Mugabe. Mlinzi wa rais huyo amemlaumu Grace kwa kitendo hicho cha kumpiga Mh Mugabe hadharani na kudai kuwa alipaswa kufanya kitendo hicho wakiwa chumbani. Kwa upande wake Grace anadai hawezi kufuata taratibu kwa kusubiria mpaka afike chumbani kutokana na ukweli kwamba yeye pia ni boss wao kwa kuwa ni mke wa rais. Read full story here...Source: NEWS SA Harare – Police deputy commissioner general and close relative of president Robert Mugabe Innocent Matibiri is being blamed for failing to protect the dictator as details emerge of the embarrassing altercation in which the president was beaten up by his wife Grace Mugabe. Footage of the incident shows Grace Mugabe slapping her husband in a fit of rage. Matibiri, Mugabe’s chief police guard, rushes in and tries to calm the situation, telling Grace Mugabe that if she wants to fight her husband she must do it in their bedroom, not in pu

LIST 10 YA GARI ZA THAMANI KUBWA WANAZO MILIKI WENYE NAZO!

Picha
List 10 ya gari za thamani kubwa wanazomiliki Mastaa wa Rap Duniani List 10 ya gari za thamani kubwa wanazomiliki Mastaa wa Rap Duniani 0 By choicetz on May 8, 2016 Burudani , News Kama ni mpenzi wakuafuatilia maisha ya mastaa wa Rap Duniani na vitu wanavyomiliki, basi hii isikupite, May 08 2016 nimekuwekea list ya mastaa wa Rap wanaopush ndinga kali na za thamani kubwa Duniani. 10. Maybach 57 ($417,402) Rick Ross 9. Spyker C8 Aileron ($500,000) Akon 8. Lamborghini Murcielago ($510,000) 50 Cent 7. Rolls Royce Phantom Drophead ($533,000) P. Diddy 6. Lamborghini Aventador ($750,000) Kanye West 5. Maybach 62 Landaulet ($1.4 million) Birdman 4.

Utumbuaji Majipu Siyo Ukatili- Rais Dkt. Magufuli Afunguka Kanisani

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema hatua anazochukua kwa ajili ya kuwasimamisha watumishi wa umma kazi zisitafsiriwe kama ni ukatili kwakuwa watumishi hao wamekuwa wakifanya mambo kinyume na maadili ya utumishi wa umma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 08 Mei, 2016 ameungana na waumini wa Parokia ya Toleo la Bwana iliyopo katika Jimbo Katoliki la Arusha kusali ibada ya Jumapili, ambapo katika salamu zake amewaomba watanzania kuendelea kuiombea nchi yao ili kazi anayoifanya ya kukabiliana na matatizo yanayowakabili watanzania wanyonge ifanyike kwa mafanikio. Dkt. Magufuli amesema hayo alipokaribishwa na Mwenyekiti wa Parokia hiyo Bw. Philemon Mushi kuwasalimu waumini wa kanisa hilo, mara baada ya kumalizika kwa ibada ya Jumapili ya kupaa kwa Bwana. "Niko pamoja na nyinyi ndugu zangu watanzania na wana Arusha wote, napenda kuwaahidi tena sitawaangusha, nitasimama mbele kuwatetea mas

Mauaji Gesti ..Meya Ataka Gesti zifungwe Kamera za Siri...

Picha
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita ameshauri kufungwa kwa kamera maalumu  za CCTV kwenye  nyumba zote za kulala wageni na hoteli ili kuimarisha ulinzi. Ushauri huo wa Mwita unakuja baada ya  siku sita  kupita , kutokea kwa tukio la mwanamke mmoja kufariki dunia akiwa gesti. Mwita ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Vijibweni (Chadema), alisema mamlaka husika wakiwamo wamiliki wa hoteli na nyumba hizo waliangalie suala hilo kwa jicho la tatu kwani litasaidia kwa kiasi kikubwa kuzuia matukio kama hayo. “Kamera hizi zisifungwe chumbani bali zifungwe maeneo ya nje  na mapokezi kwenye jingo husika.Hii ni njia sahihi ya kupambana na matukio kama haya maana hili lipo hivi linaweza kutoke lingine zaidi ya hili,” alisema Mwita ambaye alishika madaraka hayo Machi 22mwaka huu. Mbali na hilo, Mwita alisahauri pia kuboreshwa kwa mfumo usalama katika maeneo mbalimbali ili kuzuia vitendo kama hivyo vya kinyama vinavyokatisha uhai wa binadamu. Hata hivyo , Mwita  aliwaom

HII NDO SHERIA MPYA YA GUEST HOUSE DAR…Kabla ya kupewa chumba mnapigwa picha?

Picha
HII NDO SHERIA MPYA YA GUEST HOUSE DAR…Kabla ya kupewa chumba mnapigwa picha? Ijumaa ya May 6 2016 kama ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii hususani Whatsapp najua utakuwa ulipokea ujumbe ambao ulikuwa unaripotiwa kuwa umetoka kwa meya  wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita, ujumbe uliokuwa umeenea ulikuwa unahusisha kuwa meya wa Dar es Salaam Isaya Mwita ametangaza sheria mpya. Meya Isaya Mwita ameeleza kuwa ujumbe unaoenea kuwa ametangaza sheria mpya Dar es Salaam sio wa kweli na umetungwa na watu ambao wanapanga kumchafulia jina lake. Ujumbe wa uongo ambao ulisambazwa leo May 6 2016 na kudaiwa umetoka kwa meya wa Dar es Salaam “Sio kweli kuwa kuna sehemu nimetoa statement ya namna hiyo ila huyo atakayekuwa ameandika atakuwa na lengo tofauti, kwa hiyo naomba wananchi wapuuze hiyo

Mchezaji wa Azam Farid Mussa Afaulu Majaribio Nchini Hispania....

Picha
WINGA wa kimataifa wa Tanzania, Farid Mussa Malik (pichani kulia) wa klabu ya Azam ya Dar es Salaam amefaulu majaribio katika klabu ya Deportivo Tenerife ya Ligi Daraja la Kwanza nchini Hispania. Mkurugenzi wa Azam FC, Yussuf Bakhresa anayefuatilia majaribio ya mchezaji huyo Hispania, amesema kwamba CD Tenerife sasa inatarajiwa kuingia katika mazungumzo na Azam FC juu ya kumnunua mchezaji huyo. “Tunatarajia kuanza mazungumzo nao juu ya suala la Farid, ingawa wazo lao la awali ni kumchukua kwa mkopo wa miaka miwili. Sasa tunasubiri ofa yao rasmi, kisha Bodi ya Ukurugenzi itajadili na kutoa maamuzi,”amesema Bakhresa. Kwa upande wake, Farid amefurahia matokeo hayo na kusema haikuwa kazi nyepesi kwake kuweza kuwaridhisha maofisa wa benchi la ufundi la Tenerife. “Kwa kweli nimefurahi sana na ninamshukuru Mungu kwa kufuzu majaribio, ila haikuwa kazi nyepesi, mpira wa Ulaya mgumu,”amesema. Awali, Farid ilikuwa apelekwe moja ya klabu za Ligi Kuu ya Hispania, maarufu