Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2015

Mume wa Isha Mashauzi Maarufu kama Tevez akatwa Uume Sauz Afrika baada ya kuiba madawa ya Kulevya

Picha
kimewaka south jamaa aficha madawa na kudai yamepotea. wazee wakazi wafanya yao ni Tevez mume wa fatma mchina au aliyekua mume wa isha mashauzi.Ndio hivyo washakata dudu wizi umemponza alikuwa mume wa Isha mashauzi.Wauza madawa wana roho ngumu sana  

DUNIA INA MAMBO...!! HUYU KAAMUA KUINGIA NA SHELA LA HARUSI MITAANI…KISA NI WAZAZI WAKE

Picha
Mwanamke mmoja nchini  Misri  ameamua kukatiza na gauni la arusi mitaani kupinga masimango anayokutana nayo kwa kuchelewa kuolewa. Samah Hamdi   mwenye miaka 27  alifikia uamuzi huo baada ya kuchoshwa na kashfa kutoka kwa watu wanaomzunguka ikiwemo familia yake hasa mama yake mzazi ambao wamekua wakimsema  kutokana na kutokua na mume mpaka sasa.

ZITTO AMWAGA MACHOZI UKUMBINI

Picha
Hakika wikiendi iliyopita ilikuwa ni shangwe tupu, lakini kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia leseni ya Chadema, Zitto Zuber Kabwe ilikuwa ya machungu pale alipojikuta akimwaga chozi ukumbini. Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia leseni ya Chadema, Zitto Zuber Kabwe akiwa na Christian Bela. Mpango mzima ulioshuhudiwa na paparazi wetu ulijiri kwenye Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar ambapo Bendi ya Malaika, chini ya Christian Bella ilikuwa ikishusha burudani ya kufa mtu. Wakati Mbunge wa Jimbo la Sikonge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Said Nkumba alitesa kwenye jukwaa la Msondo Ngoma pale TTC Chang’ombe, Temeke, Zitto alifunika vibaya Mango Garden, Kinondoni, kwani alikuwa zaidi ya shabiki, pedeshee na mwimbaji. Katika muda ambao watoto wa mjini husema ni usiku mnene, Zitto ambaye yupo katika mgogoro na chama chake, alipanda jukwaani wakati prezidaa wa Malaika Band, Christian Bella ‘Obama’ akiimba wimbo wake mpya wa ‘Nani Kama Mama’ ambap

Huyu ndie Star kutoka South Afrika anayetoka na wema Sepetu kwa sasa....Wema Afunguka

Picha
Nimekuwekea hapa U Heard ya leo January 20, story ya leo ni kuhusu tetesi kuwa mwigizaji Wema Sepetu baada ya kuachana na Diamond Platnumz kwa sasa ana uhusiano na mwanamitindo Mtanzania anayefanya kazi zake Afrika Kusini,  Ally Daxx. Mwanamitindo Ally Dax. Gossip Cop alimtafuta Wema na kumuuliza kuhusu story hiyo kama kuna ukweli wowote, Wemaamekataa kuwa na uhusiano na mwanamitindo huyo.

Picha: Angalia Daily Mail Walivyomuumbua Balotelli

Picha
Gazeti la Daily mail limemuumbua mshambuliaji kutoka nchini Italia pamoja na klabu ya Liverpool, Mario Balotelli kwa kuanika picha zake mtandaoni, saa chache baada ya mchezo wa ligi kuu ya soka nchini England ambao ulishuhudia The Reds wakiibuka na ushindi wa mabao mawili kwa sifuri dhidi ya Aston Villa mwishoni mwa juma lililopita

HAKIKA HUYU MREMBO WA BONGO MUVI ANAPENDEZA HASWAA ...ANA SWAGA BALAA...HEBU CHEKI PICHA ZAKE 10 HAPA

Picha

HATIMAYE DIAMOND AMPACHIKA MIMBA ZARI

Picha
Baada ya sokosoko kuu la kwanini?? muda wote huu kijana Nassib Abdul – Diamond Platnumz pamoja na list yake ndeeeefu ya mabinti wa bongomovies aliowahi kutembea nao hajawahi kuwa hata na mtoto wa kusingiziwa, HATIMAYE jana kupitia kwenye nyezo za kiteknolojia tumeweza kudokezwa juu ya ujauzito alionao mwanadada  ZARI  ambao ni fika utakuwa wa kijana huyu anayetamba na wimbo wa “Nitampata wapi” ambao wachunguziwa mambo wanadai ETi ni dedication kwa mpenzi wake maarufu wa zamani.

HILI NDILO JAMBO LILILOMKUTA MSANII AY, INASIKITISHA SANA

Picha
AY ambaye kwa sasa yupo jijini Nairobi, Kenya, ameiambia Bongo5 kuwa anashangaa kugundua kuwa namba yake ya simu inapatikana wakati chip anayo yeye na haipo kwenye simu. Fundi Frank ni miongoni mwa marafiki wa AY walioombwa fedha na mtu huyo Kuna mtu amehack namba yangu ya Tigo anaomba watu pesa HIZI NI BAADHI YA TWEET ZA AMBWENE YESSAYA — Ambwene AY (@AyTanzania) January 12, 2015 Niko Kenya line yangu iko off but nashangaa huko Tanzania iko ON na inatumika — Ambwene AY (@AyTanzania) January 12, 2015 Kufuatia tukio hilo, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ameziagiza mamlaka husika kufuatilia haraka jambo hilo. “ @Tigo_TZ : @JMakamba @AyTanzania tunalipeleka swala hili kwenye idara husika lifanyiwe uchunguzi.”>>>lipatiwe ufumbuzi. — January Makamba (@JMakamba) January 12, 2015

KAMPUNI YA SAMSUNG YATANGAZA SIMU MPYA IJULIKANAYO KAMA "GALAXY A7" ITAZAME HAPA.

Picha
1. KIOO 5.5-inch super AMOLED   2. 2GB of RAM  3. 16GB storage NA INATUMIA microSD  4. LTE Category 4 5.  5-megapixel KAMERA YA MBELE  6. 13-megapixel KAMERA YA NYUMA  7. Wi-Fi  8. Bluetooth  9. NFC  10. Android 4.4.  11. 2,600 mAh battery

SIKU ZA DIAMOND KUWA NA ZARI ZINAHESABIKA

Picha
Licha ya vyombo vya habari Tanzania kuyapalilia mapenzi ya wawili hao, hali ni tofauti nchini Uganda ambako mapaparazi wamekuwa wakiibua mambo ya sirini ya msanii na mwanamama huyo tajiri nchini humo. Kikubwa kinachozungumziwa ni kuhusu tabia ya Zari kutoka na wanaume tofauti. King Lawrence, anayedaiwa kuwa mpenzi wa Zari ametangaza dau la Dola 40,000 kwa Diamond ili amwache dada huyo WASWAHILI wanasema ngoma ikivuma sana hupasuka. Msemo huu unalandana na penzi la Zari ‘The Boss Lady’ na nyota wa muziki Afrika, Diamond Platnumz, baada ya mapenzi yao kuchukua sura mpya.

WOLPER HATIMAYE AKUBALI KUPOSWA

Picha
BAADA ya msanii wa filamu hapa Bongo, Manaiki Sanga kutangaza nia ya kutaka kumposa mwigizaji Jacqueline Wolper, staa huyo ameibuka na kumjibu kuwa na yeye yupo tayari kama ataweza kutimiza masharti. Mwigizaji wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper akipozi na Manaiki. Akizungumza na mwanahabari wetu, Wolper alisema katika mila za Kiafrika, posa haikataliwi, inatolewa na kisha inajadiliwa kwa hiyo kama Manaiki kajipanga, apeleke posa ikajadiliwe na wazee wake. “Nimesikia habari za Manaiki kutaka kuniposa nikacheka sana kwa sababu yeye kama yupo tayari apeleke posa itapokelewa kwani siku zote vigezo na masharti huzingatiwa, afuate utaratibu tu,” alisema Wolper. ASANTE KWA KUPATA HUDUMA ZETU,TUNAKUOMBA BOFYA LIKE KUUNGANA NASI FACEBOOK

FRANK AMLALAMIKIA RIYAMA KUMZIBIA RIZIKI

Picha
Nyota wa filamu za Kibongo, Mohammed Mwikongi maarufu kama Frank. NYOTA wa filamu za Kibongo, Mohammed Mwikongi maarufu kama Frank, amedai kuwa msanii mwenzie Riyama Ally anamzibia riziki kiasi kwamba sasa anamsaka ili amweleze kitu gani aliwahi kumkosea. Akizungumza jijini hivi karibuni, Frank alisema anamtafuta Riyama ili aweze kumwambia ni kwa nini inakuwa hivyo kwa sababu katika filamu zote ambazo yeye anatakiwa kucheza, mwenzake huyo huwepo na ndiye anayependekeza watu watakaohusika na filamu hiyo. “Tukiacha ile filamu iliyofanyika nchini Uingereza ambayo iliandaliwa na Dida Entertainment, kuna filamu nyingine iliandaliwa na Mbunge Shamsa Mwangunga ambaye alinipigia simu na kuniomba nicheze nafasi aliyoipendekeza lakini baada ya siku, nafasi yangu ikachukuliwa na Slim. Msanii wa filamu Bongo, Riyama Ally. “Pia kuna nyingine ambayo iliandaliwa na mtu wa mtaani kwetu ambaye ni mfuatiliaji mzuri wa kazi zetu, nafasi yangu ikachukuliwa tena na Msu

PANYA ROAD 510 WATIWA MBARONI!

Picha
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Suleiman Kova  Dar es Salaam.   Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imewakamata vijana 510 wanaodaiwa kuhusika na mtandao wa uhalifu maarufu ‘Panya Road’ katika wilaya za Kinondoni, Temeke na Ilala. Mbali na hilo, wazazi na walezi wa watuhumiwa hao wameonywa kutokwenda katika vituo walivyohifadhiwa vijana wao hadi polisi itakapojiridhisha baada ya upelelezi. Januari 2, maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam yalikumbwa na taharuki kubwa kwa saa mbili baada ya kuwapo kwa uvumi wa kundi hilo kuvamia mitaa mbalimbali na kupora mali. Baada ya tukio hilo, polisi waliendesha msako mkali na kuwakama vijana 36 wenye rekodi ya kufanya uhalifu. Jana, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova alisema watuhumiwa wengine 510 walikamatwa katika maeneo mbalimbali ya vijiweni na wengine wakifuatwa katika nyumba wanazoishi baada ya polisi kupata taarifa za kiintelijensia. “Kati ya hao 510, kuna viongozi

Nani Zaidi Kwa Uzuri Kati ya Wema Sepetu na Zari The Lady Boss ?

Picha
Kwenye Mitandao ya Jamii Hasa Instagram kwa Sasa zimeibuka Team Mbili Kubwa zinazoshinda huko kwa Kupeana Vijembe vya Hapa na Pale Kuhusu Wema Sepetu na Mrembo Zari The Lady Boss wa Uganda, Ushandani huo wa Team Zari na Team Wema Umekuja Baada ya Mwanamuziki Diamond Kuwa na Mahusiano ya Kimapenzi na Wote hao wawili kwa Muda tofauti ambapo kwa sasa Diamond Ameweka Wazi Kuwa anatoka na Zari ... Ubishi mmoja wapo ni kuwa nani ni mzuri wa Umbo na Sura kati ya wema Spetu na Zari , Nasisi hatuna hiyana tumeona tuwabambanishe Hapa tuone nani atapata kura nyingi ... Haya Nani Mrembo zaidi kati ya Wema Sepetu na Zari The Lady Boss?

MAYWEATHER HII SASA SIFA, ANGALIA MAGARI ANAYOMILIKI, HADI NDEGE!

Picha
POTELEA MBALI HATA UKISEMA HII SASA NI SIFA. ANGALIA JAMANI BONDIA FLOYD MAYWEATHER ANAMILIKI MAGARI YA KIFAHARI HADI YA THAMANI YA DOLA MILIONI 5.45. PIA ANAMILIKI NDEGE, AKIAMUA ANAINUKA TU ANGANI. JAMANI....HII SASA SIFA, EEEH!

BINTI WA MIAKA 14 ALIYEUWA WATU 1000 KWA DAKIKA MOJA AKAMATWA!

Picha
Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Zahrau Babban Gida (14) ameshikiliwa na jeshi la polisi nchini Nigeria baada ya kukamatwa akiwa katika harakati za kuripua bomu kwa kujitoa mhanga.  Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii, Msichana Zahrau amekamatwa wakati alipokuwa amejifunga mabomu mwili mzima tayari kwa kufanya maangamizi na alichokuwa akikisubiri ni kuripuka tu. na kama angefanikiwa basi angeweza kutoa uhai wa watu zaidi ya 1000 kwa dakika moja tu.  Zuhrau amezungumza na vyombo vya habari akiwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi la nchini humo na kusema kuwa, amejiunga na kundi la Bokoharamu kutokana na msukumo kutoka kwa baba yake mzazi ambaye ndiye aliyemlazimisha kujiunga na kundi hilo.  Zahrau ameongeza kuwa alipofika huko kwenye kambi ya Bokoharam aliwakuta wasichana wengi ambao wamepewa mafunzo ya kujitoa mhanga.  Uchunguzi umebainisha kwamba Bokoharam wameamua kutumia watoto wadogo katika kujitoa mhanga kwasababu watu wazima wamekuw

GARI MPYA ANAYOMILIKI WIZKID INA THAMANI YA SHILINGI MILIONI 384 ZAKITANZANIA!

Picha
Wizkid anasherekea mwaka 2015 akiwa ameingiza gari mpya ndani ya yard yake ya magari, staa huyu kutoka nigeria mwenye umri wa miaka 24 amenunua gari aina ya 2015 Bentley Continental GT lenye thamani ya dollar za kimarekani $226,344 sawa na billion 384 za kitanzania, kupitia akaunti yake ya instagram aliandika hivi;  New year whip! Thankful to God: we been grinding son! Hizi ni baadhi ya picha za gari linavyoonekana!

KAULI YA BILIONEA MENGI JUU YA MTU ANAYE JIITA PROFESA....KAMPA SALAMU HII YA MWAKA MPYA

Picha

JB WA BONGO MUVI AAMUA KUJIPOTEZA!

Picha
Muigizaji mkongwe kwenye filamu nchini, Jacob Steven ‘JB’. MUIGIZAJI mkongwe kwenye filamu nchini, Jacob Steven ‘JB’ ameamua kujipoteza kwa makusudi katika uigizaji akiwa na lengo la kuweka mbele kazi zinazofanywa na kampuni yake ya uzalishaji sinema ya Jerusalemu.Akipiga stori na gazeti hili, JB alisema mwaka 2014 filamu zake tatu za Bado Natafuta, Wageni Wangu na Chausiku zilifanya vizuri sokoni.  “Kwa asilimia 80 mwaka huu kwangu umekuwa mzuri kikazi, nimefanya kazi nzuri bila mimi kuonekana kwa sababu nataka Jerusalemu ianze halafu mimi baadaye ndiyo sababu kubwa iliyofanikisha muvi zangu zote kufanya vizuri, sitaki kuwa naonekana mara kwa mara kwenye filamu,” alisema.