BINTI WA MIAKA 14 ALIYEUWA WATU 1000 KWA DAKIKA MOJA AKAMATWA!



Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Zahrau Babban Gida (14) ameshikiliwa na jeshi la polisi nchini Nigeria baada ya kukamatwa akiwa katika harakati za kuripua bomu kwa kujitoa mhanga. 
Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii, Msichana Zahrau amekamatwa wakati alipokuwa amejifunga mabomu mwili mzima tayari kwa kufanya maangamizi na alichokuwa akikisubiri ni kuripuka tu. na kama angefanikiwa basi angeweza kutoa uhai wa watu zaidi ya 1000 kwa dakika moja tu. 
Zuhrau amezungumza na vyombo vya habari akiwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi la nchini humo na kusema kuwa, amejiunga na kundi la Bokoharamu kutokana na msukumo kutoka kwa baba yake mzazi ambaye ndiye aliyemlazimisha kujiunga na kundi hilo. 
Zahrau ameongeza kuwa alipofika huko kwenye kambi ya Bokoharam aliwakuta wasichana wengi ambao wamepewa mafunzo ya kujitoa mhanga. 
Uchunguzi umebainisha kwamba Bokoharam wameamua kutumia watoto wadogo katika kujitoa mhanga kwasababu watu wazima wamekuwa wakishitukiwa kirahisi katika harakati zao. 
Chanzo: Nigernews

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA