TCRA Yadai Haipendi Kufungia vyombo vya Habari ila Sheria Inawalazimu

Mamlaka ya Mawasiliano ya Tanzania, TCRA, imesema haifurahii kuvifungia vyombo vya habari bali inavitaka vifuate kanuni na sheria zilizopo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA, Joseph Mapunda, ameyasema hayo akiwa jijini Mbeya.

“Hatufurahii vyombo kufungwa, hatufurahii vyombo kupewa adhabu,lengo kubwa ni kuvifanya vyombo viwajibike, kwa mujibu wa sheria viwajibike pia kwa wananchi,viwajibike kwa nchi,” alisema.

“Tunasajili vyombo vingi ili viweze kusaidia, kuhamasisha, kuelimisha, na kuhabarisha wananchi sasa litakuwa halina maana,” aliongeza.

Hivi karibuni kamati hiyo ilikifungia kwa miezi mitatu kituo cha redio cha Radio 5.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.