Trump awasili White House




Rais mteule wa Marekani Donald Trump amewasili katika Ikulu ya White House, kwa mujibu wa maafisa nchini Marekani.
Hata hivyo aliingia akitumia mlango tofauti na kuwasili kwake hakukunaswana kamera za waandishi wa habari.
Anatarajiwa kuwa kwenye mazungumzo na Rais Obama wakati huu.
Licha ya tofauti zao, bwana Obama siku ya Jumatano alikishauri kikosi chake kufanya jitihada zaidi kuhakisha kuwa kuna mafanikio kwenye shughuli ya kupokeza madaraka kwa Republican mwezi Januari.
Image caption Waandishi wa habari wakimsubiri Trump White House
Mapema kikosi cha kampeni ya Trump kilikutana na washauri kujadili masuala kuhusu siku za kwanza 100 za Trump kama rais na uteuzi muhimu katika nyadhifa za serikali.
Majina yaliyotajwa ni kati ya wale waliomuunga mkono Trump kutoka mwanzo akiwemo aliyekuwa spika Newt Gingrich, maseneta Jeff Sessions na Bob Corker pamoja na aliyekuwa meya wa New York Rudy Giuliani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.