NEY WA MITEGO AMPIGA BITI MRISHO MPOTO

Rapa Nay wa Mitego amedai msanii wa muziki wa asili, Mrisho Mpoto akiamua kuingia kwenye muziki wa Hip Hop atakuwa hana mpinzani kutokana na uwezo wake wa kuandika mashairi.

nay new2

Akizungumza na Bongo5 Jumanne hii, Nay alisema ikitokea akaingia labda atashindanishwa na Fid Q.

“Kwa sasa nasema Fid Q hana mwezake katika uandishi, lakini namuona Mrisho Mpoto kama angeamua kuingia kwenye Hip Hop sijui utamshindanisha na nani,” alisema Nay.
“Huyu jamaa huwa nafikiria anaumiza kichwa kiasi gani kuandaa kazi yake, anatumia akili nyingi sana ndio maana nasema kama akiingia kwenye muziki wa Hip Hop atakuwa hana mpinzani,” aliongeza.
Aidha, Nay wa Mitego amewataka mashabiki wa muziki wake kukaa mkao wa kula, kwani anajipanga kuachia kazi mpya hivi karibuni.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.