HILI NDILO TUNDU WATUHUMIWA WA UJANGILI WALIPO TOROKEA

Tundu lililotobolewa na Mahabusu hao. na kutoroka.


Watuhumiwa watatu wa kesi za ujangili pamoja na mauaji wametoroka mahabusu katika kituo cha polisi wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu, mara baada ya kutolewa mahakamani kusikiliza kesi zinazowakabili.
Tukio hilo lilitokea terehe 19/02/2016 majira ya usiku, ambapo ilielezwa kuwa walitoroka wakati mvua ikinyesha muda huo, huku wakichimba ukuta kwa kutumia kitu chenye ncha kali kutoboa ukuta wa mahabusu hiyo.
Akidhibitisha kutokea kwa tukio hilo  Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani hapa Audax Majaliwa, alisema kuwa kutokana na tukio hilo askari saba wanashikiliwa.
Majaliwa alisema kuwa watuhumiwa hao kabla ya kutenda tukio hilo, terehe 01/02/2016 walifikishwa katika mahakama ya wilaya ya Meatu ili kusikiliza kesi zinazowakabili.
Aliwataja watuhumiwa hao waliotoroka kuwa ni Chiluli Sitta (28) mkazi wa kijiji cha Mwasangula kata ya Itinje wilayani humo, ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi a mauaji.
Wengine ni Msanja Ndangule (45) pamoja na Paschal Masanja ambao ni Baba na mtoto wake, wote wakazi wa kijiji cha Sapa kata ya Itinje wilayani humo ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi ya ujangili.
Alisema katika mahabusu hiyo walikuwemo jumla ya watuhumiwa sita, ambapo watatu ndiyo walitoroka na wengine wawili walibaki, ambao ndiyo walitoa taarifa kwa askari kuwa wenzao wametoroka kwa kuchimba ukuta.
“ jambo la kushangaza kwa nini wengine walibaki? Na hao waliotoroka wanatoka kata moja…tunahofu hapa kuwa kulikuwepo na njama…lakini wale waliobaki walieleza kuwa waliona dalili mapema kwa wenzao kuwa wako kwenye mipango mikubwa” Alisema Majaliwa
 askari saba wanashikiliwa ili kusaidia uchunguzi wa tukio hilo ambao ni G 8371 PC Adam, F 9840 DC Hussen, D 5582 Copro Piter ambaye alikuwa Kiongozi wa zamu ziku ya tukio, G 4806 PC John, G 8602 PC Yassin, H 8410 PC Hery Pamoja na WP 1125 Adija.
Alisema kuwa baada ya hatua hizo kwa askari hao, taratibu nyingine za kushtakiwa kijeshi zitaendelea mara baada ya uchunguzi kukamilika.
Mpaka sasa watuhumiwa hao hawajapatikana na wanatafutwa na polisi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.