MESSI KUKUTANA NA MTOTO ALIEVUMA DUNIANI KWA PICHA YAKE YA JEZI YA MFUKO WA PLASTIKI!



MCHEZAJI BORA DUNIANI ambae huchezea Klabu ya Spain Barcelona, Lionel Messi, anatarajiwa kukutana na Mtoto wa Afghanistan ambae alipata umaarufu Duniani baada ya kupigwa Picha akivaa Jezi iliyotengenezwa kienyeji kwa Mfuko wa Plastiki wa Rangi za Argentina na Jina la Messi huku pia ikiwa na Namba 10.Mtoto huyo mwenye Miaka Mitano aitwae Murtaza Ahmadi anampenda mno Messi lakini Familia yake ya Kimaskini inayoishi Jimbo la Ghazni Jirani na Mji Mkuu wa Afghanistan, Kabul, Nchi ambayo ina misukosuko ya vita, haina uwezo wa kununua Jezi Orijino ya Staa huyo wa Argentina.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.