LADY JAYDEE AVUNJA MKATABA NA GARDNER!


HABARI mpya kutoka kwa mastaa wanaodaiwa kuvunjika kwa ndoa yao, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ na Gardner G. Habash ‘Kaptaini’, inasemekana wamevunja mkataba wa kuendesha Mgahawa wa Nyumbani Lounge uliopo Ada Estate, Kinondoni jijini Dar. 

Mbongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’. Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, wawili hao walidaiwa kufikia uamuzi wa kuvunja mkataba baada ya kuona ndoa yao inasuasua kutokana na migogoro.“Lady Jaydee au Jide alipoona mambo yanakwenda ndivyosivyo alimshauri Gardner wavunje
mkataba wa Nyumbani Lounge ili kila mmoja awe na businesses (biashara) zake. “Walimfuata mmiliki wa jengo, wakamwambia kwamba wanavunja, akawakubalia,” kilinyetisha chanzo makini. Chanzo hicho kilizidi kwenda mbali zaidi na kudai kuwa mgahawa huo kwa sasa unamilikiwa na mzungu. 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.