Mbwa ahukumiwa kifo kwa kufanya ngono na mvulana wa miaka 19, mvulana ashikiliwa


Kijana wa miaka 19 anaetoka katika jamii ya Iguosa, huko Nigeria anashikiliwa na polisi wa mji wa Edo kwa tuhuma za kufanaya mapenzi na mbwa.
Kijana huyo aliyetajwa kwa jina moja la Osagiator, anadaiwa kumpeleka mbwa huyo kwenye jengo moja ambalo halijakamilika ambapo humo alitekeleza alichotekeleza..!
Akizungumzia jinsi ambavyo kijana huyo alikamatwa, mkazi wa eneo hilo, George Ogbonmwan aliiambia 
Vanguard kuwa alimuona kijana huyo mdogo akiwa amembeba mbwa yule kama mtoto na kwa mazingira aliyoyaona akadhani kijana huyo amemuiba na ndipo alipowashitua wenzake wakaamua kumfuatilia.
Lakini kufika katika jengo hilo walimkuta kijana huyo akifanya ngono na mbwa huyo kitu ambacho kiliwashangaza na kuamua kuita polisi.
Baada ya kukamatwa, kijana huyo akiwa katikati ya umati wa watu na polisi alijitetea kuwa alikuwa anatembea barabarani na ghafla akamuona mbwa huyo akimfuatilia na ndipo akaamua kumchukua lakini hajui nini kilimuingia hadi akaamua kufanya nae kitendo hicho.
“I was walking along the street. I saw a dog following me and I carried it like a baby. I just went into the uncompleted building where I did what I did to it. I don’t know what came over me.” Alisema kijana huyo.
Mmiliki wa mbwa huyo yeye alimkataa kwa madai kuwa sasa ameshachafuliwa na ameamua kumkabidhi kabisa kijana huyo.
 “The dog has to follow him. I have nothing to do with the dog again.”
Lakini mbwa yule asiye na hatia alijikuta akipata hukumu nzito ya kifo kutoka kwa wananchi kwa kukwa uongozi wa jamii hiyo wa kimila kwa hiyo mbwa huyo ni mkosi na haramu.
Wakazi hao walidai kuwa kitendo alichokifanya kijana huyo ni kinyume cha ubinadamu na kwamba aendelee kushikiliwa na polisi na asikanyage tena katika eneo hilo.
Chanzo: Vanguard.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.