MBWANA SAMATA AMEFUNIKA; CHEKI HARUSI YAKE NA MPENZI WAKE NEIMA MGANGE!
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
Haki miliki ya pichaSAMATTA/INSTAGRAMImage captionSamatta na mkewe baada ya kufunga ndoa
Ni likizo ya kimataifa na wachezaji wenzake wengi wapo katika zamu ya kimataifa lakini nahodha wa timu ya Taifa Stars na KRK Genk Mbwana Samatta alikuwa na mipango mingine kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania.
Mshambuliaji huyo matata alitumia wakati wake mzuri wa likizo hiyo siku ya Alhamisi kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi Neima Mgange.
Sherehe ya harusi yake iliofanyika katika kijiji cha kijichi mjini Dar es Salaam ilihudhuriwa na wachezaji wenzake wa Taifa Stars akiwemo Himid Mao na Thomas Ulimwengu kulingaa na gazeti hilo.
Ilikuwa sherehe ya kufana miongoni mwa watu wa familia ya Mgange walipokutana na mshambuliaji huyo ambaye ndiye mchezaji wa kwanza kutoka Tanzania kushiriki katika ligi ya mabingwa Ulaya.
Maelezo kuhusu uhusiano wa Mbwana na Neima yalikuwa ya siri kubwa na ni watu wa familia zote mbili pekee waliokuwa wakielewa kilichokuwa kikiendelea hadi siku ya Alhamisi.
Mshambuliaji huyo hakushirikishwa katika mechi ya kimataifa ambayo Taifa Stars inacheza dhidi ya Uganda wikendi hii.
Alikuwa akiugua jeraha lakini akashirikishwa katika kikosi cha timu ya Genk kilichopoteza 6-2 dhidi ya klabu ya Salzbourg kutoka Austria katika michuano ya kombe la mataifa bingwa Ulaya.
Pia aliisaidia Tanzania katika michuano ya kimakundi ya kufuzu kwa kombe la dunia Qatar 2022.
Kwanini Mbwana Samatta ananganganiwa na klabu England
Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGESImage captionMbwana Ally Samatta huchezea KRC Genk ya Ubelgiji
Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta anang'ang'aniwa na klabu tatu za England, taarifa za vyombo vya habari nchini Uingereza zinasema.
Tetesi zinasema nyota huyo anatafutwa na West Ham United, Everton na Burnley.
Samatta, 25, maarufu kwa Watanzania kama Samagoal ameng'aa sana akichezea klabu ya KRC Genk nchini Ubelgiji.
Amefungia klabu hiyo mabao 11 katika mechi 16 ambazo amewachezea msimu huu, nusu ya mabao hayo akiyafunga barani Ulaya.
Taarifa za kumhusisha Samatta na klabu ya Everton zimetoka kwa mtandao wa hitc.com, mmoja wa mitandao ambayo imeibukia kuwa maarufu kwa taarifa za wachezaji na kuhama kwao.
Kwa nini anahusishwa na Everton?
Samatta, mwenye kimo cha futi 5 inchi 11, amefunga mabao sita katika ligi ndogo ya klabu barani Ulaya, Europa League, na ni hapo ameanza kuonekana na klabu za England.
Mnamo 23 Agosti 2018 Samatta, alifunga 'hat-trick' dhidi ya Brøndby IF katika Europa League kwenye mechi ambayo walishinda 5-2.
Everton wametatizika kumpata mshambuliaji wa kutegemewa tangu nyota wao Romelu Lukaku alipowaacha na kuhamia Manchester United kwa £75 mwaka 2017.
Picha zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao kuonyesha ufahari wa hali ya juu wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa dar es salaam. Ofisi hiyo imekuwa tofauti kabisa na ile ya Mkuu wa mkoa aliyepita bwana Sadick, ofisi ya Makonda ina kompyuta kadhaa za apple,mapambo mengi ya kila aina yanayoashiria ufahari na utukufu wa hali ya juu kuliko hata ofisi ya rais. Nani aligharamia ufahari huu wakati hata ikulu haijabadili muonekano? Kulikuwa na umuhimu wa kuweka ufahari huo katika kipindi hiki cha kubana matumizi? Nini kilipungua katika ofisi ya aliyekuwa Mkuu wa mkoa mpaka ufahari uongezwe katika jiji ambalo limezungukwa na wananchi wenye hali ngumu na maisha yasiyoridhisha. By iparamasa
Haki miliki ya picha Image caption Mabaki ya ndege yalipatikana yakiolea katika eneo ambalo ndege hiyo ilitoweka siku ya Jumatatu. Maafisa wa Chile wanasema kwamba wamezuia mabaki yanayoaminika kutoka katika ndege ya kijeshi iliotoweka siku ya Jumatatu. Wanasema kwamba mabaki hayo yalipatikana yakiolea kilomita 30 kutoka eneo ambalo ndege ya wanahewa wa Chile aina ya C-130 Hercules inayobeba mizigo ilikuwa na mawasiliano ya mwisho. Vifusi hivyo vilipatikana katika maji yanayojulikana kama mkondo wa Drake. Wengi wahofiwa kufariki baada ya ndege kuangukia nyumba DR Congo Hili ndilo taifa hatari zaidi kusafiri kwa ndege? Siri yafichuliwa kuhusu mfumo wa oksijeni wa Boeing 787 Ndege hiyo ilikuwa imetoka mji wa kusini wa Chile wa Punta Arenas ikielekea katika kambi ya kijeshi ya Antarctica ambapo rais wa taifa hilo Eduardo Frei Montalva alikuwa. Vifusi hivyo huenda vinatoka kutoka tangi la mafuta la ndege hiyo , kulingana na kamanda wa jeshi la wanahewa Eduardo Mosqueira ...
Maoni
Chapisha Maoni