Chuji aenda na maji, Kaseja kazi ipo

Chuji.PICHA|MAKTABA 
  • Lakini kipa Juma Kaseja bado shughuli yake ni pevuShare
YANGA imemwondoa rasmi kiungo wake, Athuman Idd ‘Chuji’ katika kikosi hicho kitakachoshiriki msimu ujao wa Ligi Kuu Bara ambacho sasa ni rasmi kwamba kitakuwa chini ya Mbrazili,Marcio Maximo.
Lakini kipa Juma Kaseja bado shughuli yake ni pevu.
Kaseja amebakiza mkataba wa mwaka mmoja na nusu, uamuzi wake bado haujatolewa lakini anaweza kubaki.
Uamuzi wa Chuji ulitolewa katika kikao cha viongozi hao kilichofanyika Ijumaa na Jumamosi kwa madai yao ya awali kuwa mchezaji huyo ana utovu wa nidhamu ambao utawasumbua.
Habari za ndani ambazo Mwanaspoti imezipata ni kwamba  Chuji aliitwa na kupewa onyo kali akitakiwa kujirekebisha tabia huku ikielezwa kwamba kocha mpya atakayeingia mkataba na Yanga ndiye atatoa uamuzi wa mwisho juu ya kiungo huyo.
Lakini tayari uamuzi umetolewa kabla hata Maximo ambaye enzi akiwa kocha wa Taifa Stars alionyesha misimamo ya waziwazi wa kutovutiwa na tabia za Chuji.
“Chuji ana mkataba na Yanga, lakini tumekubaliana kwamba atalipwa fedha zake za kuvunjwa mkataba wake, bado hajapewa taarifa Chuji ila ukweli upo hivyo atapata timu nyingine kwani zipo nyingi.
“Hata viongozi wenyewe waligawanyika kuhusu Chuji kuna waliotaka abaki na wengine hawahitaji, hivyo maamuzi ya mwisho ni kumwondoa kikosi,” alisema kiongozi huyo ambaye alitaka jina lake lihifadhiwe mpaka hapo viongozi watakapotoa taarifa rasmi ya wachezaji watakaoachwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

SASA HII NI NGONO BONGO MUVI.... Video ya Irine Uwoya na Rich wakifanya YAO..LIVE

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

BEIJING DAXING: UWANJA MKUBWA WA KIMATAIFA WA NDEGE CHINA WAFUNGULIWA, HATARIIII!