Breaking News Wakurugenzi wote wa NSSF wamesimamishwa kazi, kupisha uchunguzi wa idara zao katika shirika hilo.


BODI ya wakurugenzi ya Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limewasimamisha kazi wakurugenzi sita na meneja watano na Mhandisi mmoja kufuatia matumizi mabaya ya ofisi na kutofuata sheria na kanuni.

Kwa mujibu wa taafia iliyotolewa leo na Mkurugnezi Mkuu wa NSSF,  Profesa Godius Kahyarara imesema hatua ya kuwasimamisha kazi wakurugenzi na mamenja hao inafuatia kikao cha bodi chini ya uenyekiti wa  Prefesa Samweli Wangwe kilichokaa kuanzia Ijumaa iliyopita.

“Bodi imeagiza  kusimamishwa kazi Wakurugenzi , Mameneja watano na Mhandishi mmoja ili kupisha uchunguzi ili kubaini wahusika katika tuhuma za ubadhirifu, matumizi mabaya ya ofisi na kutofuata kanuni, sheria na utatibu katika uwekezaji,  usimamizi wa miradi na manunuzi ya ardhi na ajira,” alisema Profesa Kahyarara.

Aliwataja wakurugenzi hao ni Mkurugenzi wa mipango, Uwekezaji na Miradi, Yakub Kidura, Mkurugenzi wa fedha, Ludovick Mrosso, Mkurugenzi wa rasilimali watu na utawala, Chiku Matessa, Mkurugenzi wa Udhibiti,Hadhara na Majanga, Sadi Shemliwa, Mkurugenzi Mahesabu ya ndani, Pauline Mtunda na Mkurugenzi wa Uendeshaji,  Crescentius Magori.

Aidha Aliwataja mameneja waliosimamishwa ni pamoja na Meneja wa utawala, Amina Abdallah, Meneja wa Uwekezaji, Abdallah Mseli, Meneja Miradi, Mhadisi,John Msemo, Mhasibu Mkuu, Davis Kalanje, Meneja kiongozi mkoa wa Temeke, Wakili,  Chedrick Komba na Mhadisi John Ndazi.

Awali amedaiwa kuwa baadhi ya wakurugenzi na mameneja waliosimamishwa, leo wamefikishwa katika kituo cha polisi cha kati Dar es Salaam kwa mahojiano kufuatia tuhuma hizi zinazowakabili.

a wakurugenzi wote wa NSSF wamepigwa chini leo na wanne kati yao wako chini ya ulinzi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.