SIKIA HII! Samsung yakiri Tv zao zinanasa sauti.


Samsung imewaonya wateja wake kuhusu kutojadili mambo yao ya kibinafsi mbele ya televisheni zao
Samsung imewaonya wateja wake kuhusu kutojadili mambo yao ya kibinafsi mbele ya televisheni zao.
Onyo hilo ni kwa wale watazamaji ambao hudhibiti televisheni zao kwa kutumia sauti.
Baadhi ya runinga hizo za kisasa husikiliza mambo ambayo wanasema na zinaweza kuwasilisha ujumbe kwa Samsung au mashirika yanayohusiana na Samsung kibiashara..
Onyo hilo limetolewa baada ya habari kuchapishwa katika gazeti la mtandao "Daily Beast" iliyochapisha sehemu ya sera za Samsung zinazosimamia umiliki wa kibinafsi wa televisheni zao.
Sera hiyo inaelezea kwamba televisheni hizo zitakuwa zinasikiliza watu katika chumba kimoja wakijaribu kutoa amri na maswali kutumia vibonyezi.
''Iwapo maneno ambayo umeyatamka ni ya kibinafsi au ya kisiri , basi ujue kuwa habari hiyo itakuwa kati ya habari zilizonaswa na kusambazwa kwa watu wengine.'' Samsung imeonya.
Televisheni hiyo inaweza kunasa sauti
Kutokana na kukabiliana kuhusu taarifa ya sera yake ,Samsung imetoa taarifa kufafanua jinsi sauti hizo zinavyofanya kazi.
Inasisitiza utambuaji wa sauti unajulikana tu baada ya mmiliki kuchagua kutumia sauti badala ya kubonyeza kifaa cha kiungia mbali (remote control)
Samsung imesema kama mteja atakubali kutumia kifaa cha kugundua sauti, sauti hiyo itatambuliwa na mtu wa upande wa tatu baada ya amri ya kuitafuta sauti hiyo.
Upande watatu ambao unatafsiri sauti kutoka kwa wamiliki hufasiriwa na kampuni inayoitwa Nuance, ambayo imehitimu kutambua sauti.
Samsung si kampuni ya kwanza kujipata mashakani kwa kutumia vinasa sauti kwenye mashine na bidhaa zake.
Mwishoni mwa mwaka wa 2013,mshauri wa maswala ya kiteknolijia kutoka Uingereza aligundua kuwa televisheni yake ya LG ilikuwa inakusanya habari kuhusu tabia yake ya utazamaji wa televisheni.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Ujerumani yanyakua Kombe la nne la Dunia

Abu Bakr al-Baghdadi: Nguo ya ndani ya kiongozi wa IS 'iliibiwa' kufanya uchunguzi wa DNA

HILI NDILO BIFU KUBWA KATI YA RIHANA NA NICK MINAJ.