Machapisho

AFISA TARAFA WA KIBITI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MWANAFUNZI WA DARASA LA SITA

Picha
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Boniventura Mushongi akizungumza na waandishi wa habari kuhusina na tukio la kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa Afisa Tarafa wa Kibiti kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa darasa  la sita katika shule ya Kitunda.(Picha na Victor Masangu) NA VICTOR MASANGU,  PWANI JESHI la  polisi Mkoa wa Pwani limemkamata na kumfikisha mahakamani  Afisa Tarafa wa Kibiti Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani Selemani  Mpangile almaarufu babu konyeza kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa darasa la sita  katika shule ya msingi kitunda. Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi  ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Boniventura Mushogi amesema kwamba tukio hili limetokea juzi majira ya saa 10 jioni ambapo mtuhumiwa aliamua kutenda kosa hilo kinyume na sheria na  taratibu za nchi. ...

Gari Aina ya Toyota Hiace Lililozama Majini Kivuko cha Kigamboni na Kuua Watu Wawili Lapatikana

Picha
Lile Gari Aina ya Toyota Hiace lililozama kwenye bahari kivukoni Kigamboni na kuuwa watu wawili limepatikana na kutolewa majini na wana maji baada ya Jumatano ya April 20 2016 kuzama  ikiwa na watu wa wawili ambao wote walipatikana wakiwa wameshafariki... Picha likiwa linatolewa majini hii hapa: Hatimaye kikosi cha ukoaji cha baharini kimefanikiwa kuitoa gari aina ya Hiace ambayo jana ilizama katika bahari ya hindi eneo la Kivukoni na kuua watu wawili.

Watu Wanne Watiwa Mbaroni Sengerema Kwa Kunywa Pombe Mchana

Picha
Wilaya ya Sengerema imeanza kutekeleza kwa vitendo agizo la Rais baada ya kukamata watu wanane waliokutwa wakinywa pombe saa za kazi. Amri ya kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa watu hao ilitolewa juzi na Mkuu wa Wilaya Zainabu Terack baada ya kukuta baa zimefunguliwa asubuhi zikiwa na wateja waliokuwa wakipata kinywaji kabla ya saa 9:30 alasiri, muda ambao ofisi za Serikali hufungwa. Rais John Magufuli alitoa agizo hilo la kupiga marufuku unywaji pombe na uchezaji pool nyakati za kazi wakati alipokuwa akiwaapisha wakuu wa mikoa mwezi uliopita. Alitaka vijana ambao watakaidi maelezo ya kuambiwa, nguvu itumike kuwalazimisha kufanya kazi. Kwa mujibu wa mkuu huyo wa wilaya, aliyeongoza oparesheni ya dakika 45 ya kusaka wanaokunywa pombe na kucheza pool muda wa kazi, watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani kwa makosa ya uzembe na kukiuka amri halali ya serikali. Wakijitetea baada ya kutiwa mbaroni, baadhi ya waliokamatwa walidai kuwa walienda baa k...

Diamond Platnumz, Mrisho Mpoto Walivyotajwa Bungeni Leo

Picha
Kikao cha tatu cha mkutano wa tatu wa Bunge la 11 kimeendelea tena Dodoma leo April 21 2016 , shughuli nzima iliyoanza asubuhi ni maswali na majibu kwa Waziri Mkuu, Pia baadhi ya Wizara zilihusishwa katika maswali hayo, ambapo Mawaziri na Manaibu Waziri wa Wizara hizo walilazimika kuyatolea majibu. Baadhi ya Wizara hizo ni pamoja na Wizara ya Habari,  Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambapo swali lililoulizwa na Mbunge wa Kasuru Mjini Daniel Nsanzugwanko ilikuwa ‘Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwekeza kwakiwango kikubwa katika Mkoa wa Kigoma kwa kujenga jumba la sanaa ili vijana wawe na sehemu nzuri ya kujiendeleza kisanaa?’ Swali la pili likawa ‘Kama Serikali inakubaliana na hoja hiyo, kituo hicho kitaanza kujengwa lini?’ Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akajibu ‘Wizara yangu inatambua mchango mkubwa wa wasanii wenye asili ya mkoa wa Kigoma kama vile Diamond, Alikiba, Banana, Mrisho Mpoto na wengine‘ ‘Wizara yangu inae...

Tetesi ya Siri Nzito Kati ya Diamond na Mrembo Aliyecheza Kwenye Video ya Raymond Kwetu Hii Hapa

Picha
Kupitia Mtandao wa Instagram Siri Nzito nzito zinaendelea kuwekwa wazi kuwa kuna siri nzito kuwa Mwanamuziki Diamond Platnumz anatoka na mrembo Officiallyyn ambaye ameonekana kwenye video ya Msanii mpya wa WCB Raymond kwenye wimbo wake Kwetu....Chanzo cha habari hii kinasema Diamond na Msanii huyo walianza kutoka muda toka mwaka jana...Inasemekana imefikia mpaka mrembo huyo amejichora Tattoo ya Simba mgongoni kwake ambalo ni jina la analojiita Diamond.. Inasemekana Mrembo huyo Lyyn kwa Sasa anapokea michambo ya nguvu na Vitisho kutoka kwa Team Zari huku...Moja ya Kitisho ni Hichi hapa Chini kutoka Instagram Wakati wengine wakirusha madongo kwa Diamond na Mrembo huyo Wengine wanampongeza Diamond kwa kuopoa kitu kizuri.... Soma Huyo Alichoandika: Nataka_shari  "UMEJUA KUCHAGUA Asanteeeeeee @diamondplatnumz c kwa uchaguzi huu kabla hujampata huyu ndo MZURI uliyemmiss kwa hawarakikongwe unakuza tuu mtoto wa jirani yetu_ila mnambemenda mtoto we unapiga mam...

Video: Rais Magufuli Awajibu Haki za Binadamu, Asema Nao Wanaweza Kuwa Majipu Kwa Kutetea Maovu....

Picha
Katika hali inayoonyesha kuwa na majibizano kati ya Rais Magufuli na Kituo Cha Haki za Binadamu LHRC kinachoongozwa na Dr. Hellen Kijo Bisimba, leo Rais Magufuli hadharani kasema wanaosema amekiuka haki za binadamu kumsimamisha ndugu Kabwe hadharani walitakiwa pia waseme vivyo hivyo kipindi anamuapisha hadharani kwa kuwa ni mteule wake, Amesema hao Waliotumbuliwa wamewaibia Watanzania hadharani hivyo inabidi watumbuliwe hadharani nao wapate maumivu kama waliyoyapata Watanzania...Hivyo, ni vyema wakaiacha serikali ikafanya kazi yake, na ikiwezekana itabidi awachunguze hao LHRC credibility yao kama wanatetea mambo maovu inawezekana nao ni majipu..

Idadi ya Watumishi Hewa Waliomfukuzisha Kazi Anne Kilango Shinyanga Yafika 226

Picha
Idadi ya wafanyakazi hewa katika mkoa wa Shinyanga ambao awali ulidaiwa kutokuwa na wafanyakazi hao kabisa, imeongezeka na kufikia 226. Hayo yamebainishwa leo na Rais John Magufuli katika uzinduzi wa Daraja la Kigamboni, ambapo alisisitiza kuwa serikali yake haitawafumbia macho viongozi ambao kwa namna moja au nyingine wataruhusu mianya ya ubadhirifu wa fedha katika maeneo yao. ”Mkoa wa Shinyanga kwa taarifa nilizonazo hadi sasa wameshapatikana wafanyakazi hewa 226 kutoka ‘zero’ hivyo ni lazima tuwajibike kwa watanzania wanyonge,” amesema Rais Magufuli. Wakati wa kuwasilisha ripoti ya Mikoa Serikalini aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela alisema mkoa wake hauna mtumishi hewa hata mmoja jambo lililopelekea Rais Magufuli kuunda tume iliyobaini watumishi  hewa  45 katika awamu ya kwanza. Baada ya kubainika uwepo wa watumishi hao, Raisi alitangaza kutengua uteuzi wa Mkuu huyo wa Mkoa kwa kutokuwa makini na taarifa anazopewa na wasaidi...